This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Thursday, July 23, 2009

Ni zamu ya Joshua John Mlelwa kung'ara






(Joshua John Mlelwa akiwa kwenye jukwaa pamoja na Kundi la Kijitonyama Upendo Group katika moja ya matamasha ya Injili yaliyofanya nchini Tanzania.

Na Mdau wetu

MAKUNDI mengi ya muziki wa Injili nchini Tanzania yamekuwa ni nguzo muhimu katika kulea vipaji vya waimbaji wengi wa muziki huu. Joshua John Mlelwa ni miongoni mwa vipaji vingi hapa nchini vilivyokulia kwenye mikono ya kundi.
Kabla ya kutoka kama muimbaji binafsi, Joshua amekuwa kwenye Kundi la Kijitonyama Upendo Group (KUG) tangu mwaka 1999.
Kabla ya kuwemo kwenye kundi hilo Joshua alikuwa akiimba kwenye Kwaya ya Vijana ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Sumbawanga mwaka 1992 na wakati huo alikuwa akisoma shule ya sekondari ya Mazwi iliyopo mkoani Rukwa.
Baadhi ya kazi alizofanya pamoja na KUG ni pamoja na Mungu Anakupenda ambayo ilikuwa ni albamu yenye nyimbo tisa ndani yake ambazo ni Haleluya, Njooni Kwangu, Tutapataje Kupona na nyingine nyingi.
Pia waliweza kutoa albamu iitwayo Maombolezo iliyokuwa na nyimbo nane, na hii waliitoa wakati wa kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, iliyokuwa na nyimbo kama Taifa Lako Lakulilia, Tutakukumbuka sana pamoja na Mbona Mapema.
Licha ya kupata mafanikio hayo akiwa ndani ya Kijitonyama Upendo Group, ametoka na albamu mbili. Albamu ya kwanza ameitoa mwaka 2007, iitwayo Yesu Yupo yenye vyimbo nane ambayo ameitoa maalum kwa ajili ya kituo cha kulelea watoto Yatima cha Hananasifu Wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.
“Unajua ukitaka kufanikiwa ni lazima uhakikishe kuwa unakuwa mtoaji ndiyo maana mimi na mke wangu tuliamua kuwa watoaji kwa kutoa albamu hii kwa gharama zetu na mauzo yote kukiachia kituo hicho bila kuchukua hata shilingi moja,” ameongeza muimbaji huyo.
Baada ya kutoka na albamu ya kwanza Joshua Mlelwa ametoka na kazi mpya iitwayo Shaloom yenye nyimbo nane ambazo ni Shaloom, Apewe Sifa Bwana, Niko Juu, Heri Niwe na Wewe pamoja na nyingine nyingi.
“Baada ya albamu ya kwanza hivi sasa nimeshatoa albamu ya pili iitwayo Shaloom na kazi hii nimeifanya ndani ya studio za Shekinah za jijini Dar es Salaam na itakuwa mtaani juma hili,” amefafanua muimbaji huyu mkongwe kwenye muziki wa Injili.
Juu ya mwelekeo wa Muziki wa Injili hapa nchini Joshua ametanabaisha kuwa mwelekeo si mbaya ila wapo baadhi ya waimbaji wa muziki huo wanaoufanya bila kuwa na hofu ya Mungu.
“Watu wanaimba bila kuwa na hofu ya Mungu, wanafanya hivi kwa kuwa wana kipaji lakini hii si sababu ya kuwa mwimbaji wa Injili kwani muziki huu unafanywa kwa ajiliya Mungu. Kwa mfano, hata Michael Jackson amekuwa maafuru ulimwenguni kutokana na kipaji chake cha kuimba lakini hakuwa na hofu ya Mungu, ” amefafanua Joshua ambaye ni baba wa mtoto mmoja.
Kuhsu suala la wizi kwenye sanaa ya Tanzania kwa ujumla, Joshua amesema kuwa ili kulikomesha tatizo hili ni kwa wapenzi wa sanaa kuachana na tabia ya kununua bidhaa bandia na wasanii kuwa na umoja na kushirikiana.
“Wizi bado ni tatizo, kwa mfano nchi nyingi za Afrika Mshariki na Kusini wanatufahamu vema kutokana na kazi zetu ambazo mapato yake hatuyaoni kwa sababu ni kazi za kunakili kutoka kwenye ‘original’,” amesema Joshua.
Baadhi ya nchi ambazo kazi za Kijitonyama Upendo Group zinauzwa kinyemela bila kuwanufaisha ni Malawi, Zambia, Kenya, Botswana, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi na Rwanda.

GAMA WAUSHUKIA MUZIKI WA INJILI




MNENDO wa muziki wa Injili kukubalika kwa mashabiki na wapenzi wake kwa sasa unachangiwa na mambo mbalimbali ambayo ni uimbaji, utunzi na utayarishaji ulio bora.
Gamaliel Daniel Mwasumbi ni miongoni mwa waimbaji ambao wamewezesha suala la uimbaji Tanzania kubadilika na kuwa wa aina yake kwa kuwa wakati anaanza kazi hii yeye na wenzake, Godwin Gondwe na David Robert waimbaji binafsi walikuwa wachche hivyo kujikuta wakiwa na mzigo wa kuhakikisha injili inawafikia watu wengi zaidi.
Katika mazungumzo yake na mdau wa tanzaniacelebrity.com Gamaliel ambaye wengine wanamtambua kama Gama anasema kuwa kwenye huduma hii ya uimbaji baadhi ya mambo hayaendi sawa hivyo kuna haja ya kuwa na neon la uponyaji kwa ajili ya waimbaji na watayarishaji wa muziki wa Injili.
Mambo ambayo Gama anayaona kama ni kikwazo kwenye muziki wa Injili ni pamoja na baadhi ya waimbaji kufanya huduma ya Injili kwa kulenga pesa badala ya kumtumikia Mungu kama ilivyokuwa hapo awali.
“Misingi ya awali kwenye uimbaji wa nyimbo za Injili umevunjwa, kwa maana zamani uinjilisti kwa njia ya uimbaji ilikuwa ni kazi ya wito lakini kwa sasa nashangaa eti muimbaji anaitwa mahali anaanza kuweka masharti mbalimbali ikiwemo suala la kutaka kulipwa,” amesema muimbaji huyo.
Kadhalika Gama ameelezea juu ya utunzi bora wa mashairi kwa kusema kwamba muziki wa Injili si mipasho hivyo waimbaji wanatakiwa kutunga nyimbo zitakazookoa roho za watu kwani hiyo ndiyo kazi ya muziki huo katika jamii.
Amefafanua kuwa kamwe Mungu hana hasara kwa maana amejitosheleza na hivyo kama watu watashindwa kuimba katika roho na kweli ataendelea kuwa Mungu.
“Waimbaji tuzingatie huduma kwa kutunga nyimbo zitakazoweza kuokoa roho za watu kwani bila kufanya hivyo mwisho wa siku tutadaiwa, lakini ninachopenda kuongezea ni kwamba kamwe Mungu hana hasara kama tukiacha kumuimbia, vile vile tusiimbe mipasho,” ameongeza Gama.
Wakati huo huo Gama ameeleza kuwa watengenazaji wa muziki huo kwenye studio (producers) wamekuwa hawaangalii ubora bali fedha imekuwa ni kichocheo kikubwa katika kufanya kazi, jambo linalochangia kutoa kazi zilizo chini ya kiwango.
Licha ya hali hiyo Gama ameongeza kuwa baadhi ya watangazaji kwenye vituo vya redio na televisheni za Kikristo wamekuwa wakiendekeza vitendo vya rushwa kwa waimbaji jambo linalosababisha wale wasiokuwa na uwezo wa kifedha kazi zao kushindwa kusikika kikamilifu.
Gama ambaye kwa sasa anakuja na albamu ya peke yake baada ya kufanya kazi na waimbaji wenzake kwenye Kundi la Yahweh Music linaloundwa na David Robert, Godwin Gondwe pamoja na yeye Gama, amesema kuwa kazi yake hii itakuwa ni tofauti kutokana na kujaza vionjo vya sehemu mbalimbali duniani.
“Albamu yangu mpya itakuwa na mchanganyiko wa vionjo vya Kihindi na Kisenegal na imepewa jina la Usinipite na ina jumla ya nyimbo 12 ambazo ni Mwenye Enzi, Mungu Mkuu, Tunakutukuza, Usinipite, Usisahau, Amen na nyingine,” ameeleza Gama.
Kabla ya kutoka kivyake Gama aliyekuwa kwenye Kundi la Yahweh Music yeye na wenzake walitoa na albamu iitwayo Baba iliyotoka mwaka 2003 na ilikuwa imebeba jumla ya nyimbo 10 ambazo baadhi yake ni Baba, Haleluya Hosana, Nakupenda, Bwana Atafanya Njia na nyinginezo nyingi.
Baadaye alienda jijini Nairobi nchini Kenya akifanya shughuli za muziki wa Injili pamoja na masomo na hivi sasa amerejea nyumbani akiwa na mke aitwaye Rose Boke pamoja na mtoto mmoja wa kiume aitwaye Ntimi.
“Napenda kuwashukuru wadau mbalimbali waliowezesha mimi kufika hapa na wanaendelea kukuza muziki wa Injili hapa nchini, nao ni Eric Shigongo Mkurugenzi wa Global Publishers, vyombo vya habari pamoja na wadau wengine,” amesema Gama.

Wednesday, July 22, 2009

mdau Seppy


Mdau Seppy (kushoto) akiwa na mdau mwenzake wakiendeleza libeneke la mikono's. Seppy ni mmoja wa wadau waliopiga nondo pale VOSA SEKONDARI MIAKA ILEE AMBAPO KWA SASA INAJULIKANA KAMA DAR ES SALAAM CHRISTIN SEMINARY, wakati huo kulikuwa na wadau kama Peris Majura, Kakore, Evelin Komu, Grace Sewe Decha kwa sasa ni waifu wa mtu, Hilda Silas naye ameuaga ukapera juzi juzi tu, du! kweli tumetoka mbali naomba tuwasiliane...!.

Voda yalamba Bingo



Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Dietlof Mare kiasi cha dola za kimarekani milioni 90 na Citi benkire(kushoto) akisaini mkataba wa mkopo waliokopeshwa na CITI benki kiasi cha dola za kimarekani milioni 90.(kulia)Ofisa Mtendaji Mkuu wa Citi Benki Naveed Riaz.



Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Dietlof Mare(kushoto) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa CITI Bank Naveed Riaz(kulia) wakibadilishana nyaraka za makubaliano ya mkopo baada ya CITI Bank kuikopesha Kampuni Vodacom Jijini Dar es Salaam.(Picha kwa hisani ya BLOG YA FULLSHANGWE)

Monday, July 20, 2009

Jinsi Maxell alivyotua Barca

Barcelona, Hispania

Harakati za usajili wa Ligi Kuu nchini barani Ulaya zinaendelea ambapo kumekuwepo kwa taarifa za hapa na tale juu ya uhamisho wa wanasoka kutoka klabu moja na kwenda klabu nyingine.

Kwa muda sasa klabu ya Barcelona mabingwa wa Ligi ya Hispania ‘La Liga’ ambao pia ni mabingwa wa Ulaya, wamekuwa katika mbio za kuweza kumnasa mlinzi wa pembeni wa kutoka klabu ya Inter Milan huku mengi yakisemwa juu ya mbio hizo.


Lakini pamoja na maneno na minong’ono mingi hatimaye wiki iliyopita mabingwa hao waliweza kunasa saini ya Maxwell Scherer Cabelino Andrade anayecheza nafasi ya ulinzi na kiungo.

Maxwell raia wa Brazil amekuwa ni miongoni mwa wachezaji waliotingisha usajili wa Ulaya kutokana na mvutano ambao ulianza jitokeza baada ya Barcelona kutoa taarifa za kumtaka.

Mchezaji huyo inasemekana kuwa anachukua nafasi ya Sylvinho, anayetarajiawa kutua kwenye klabu ya Deportivo La Coruna kufuatia kuanza mazungumzo ya chini kwa chini kati ya klabu hiyo na Barcelona.


Hata hivyo taarifa kutoka ndani ya klabu ya Barca zilisema kuwa klabu hiyo na Inter Milan wamekubaliana katika masuala yote ya uhamisho na ndiyo sababu ya mlinzi huyo kusaini mkataba wakali hao wa Camp Nou na ameshatambulishwa kwa mashabiki wa klabu hiyo ya jijini Barcelona.

Uhamisho wa Maxwell Scherer Cabelino Andrade umeigharimu Barcelona kiasi cha Pauni za Uingereza milioni saba, huku mlinzi huyo akionekana mwenye furaha kuujiunga na wakali hao wa Ulaya.

“Hii ni hatua mpya katika historia ya maisha yangu, nimekuja hapa lakini nikiwaacha marafiki, mashabiki wangu Inter Milan lakini sina budi kukubaliana na hali ya dunia, ila ninachoomba kutoka kwa mashabiki wa soka ni umoja, upendo mshikamano na mimi nitafanya kazi kwa nguvu na juhudi zote,” amesema mkali huyo.

Baadhi ya wadadisi wa masuala ya soka nchini Hispania wanasema kuwa Maxwell (27) anaweza kuwa nguzo muhimu kwenye maendeleo kwenye klabu hiyo Barcelona ambayo kwa sasa wameshikilia mataji matatu makubwa ambayo ni Kombe la Ulaya, Ubingwa wa La Liga na Copa del Rey.

Klabu ya Real Madrid ndiyo inayotingisha dunia kwa sasa kwenye usajili kufuatia kutenga kitita cha Pauni za Uingereza milioni 200 ili kufanikisha zoezi hilo huku ikifanikiwa kumtwaa Ricardo Kaká, Raul Albiol, Cristiano Ronaldo na Karim Benzema.

Maxwell Scherer Cabelino Andrade alizaliwa Agosti 27 mwaka 1981 katika eneo la Vila Velha nchini Brazil.

Kabla ya kutua Barcelona alikuwa akikipiga kwenye klabu ya Inter Milan ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Italia (LIGUE) akicheza nafasi ya mlinzi wa kulia pamoja na kiungo, pia amezitumia timu za Cruzeiro, Ajax, Empoli.