This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Monday, January 30, 2012

Hongera Twiga Stars kutuvisha Nguo

Wachezaji wa Twiga Stars kutoka kushoto ni, Mwanahamisi Omari, Etoe Mlenzi na Pulkaria Charaji wakishangilia ushindi wa timu yao.
Kikosi cha timu ya taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’ kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo wao na timu ya Namibia wa kufuzu Fainali za Mataifa Afrika kwa Wanawake (AWC) uliofanyika Jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Twiga Stars imeshinda 5-2.

Dk Harrison Mwakyembe,Samwel Sitta, Anne Kilango Malecela na James Lembeli Washiriki Misa Maalum Kanisa La Ufufuo na Uzima Lilopo Kawe Jijini Dar es S

Naibu Waziri Wa Ujenzi Dk Harrison Mwakyembe akishuka katika madhabahu mara baada ya kumalizika kwa ibada hiyo Jana
Waziri wa Afrika Mashariki Mbunge wa Urambo Samwel Sitta na akishuka katika madhabahu mara baada ya kumalizika kwa ibada jana
Waziri wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Urambo Samwel Sitta akiongea katika ibada hiyo na kumkaribisha Dk Harrison Mwakyembe ili kuzungumza machache na waumini wa kanisa hilo na kutoa ushuhuda wake.
Mbunge wa Kahama Bw. James Lembeli kushoto , akizungumza na Dk. Harrison Mwakyembe wakati wa ibada hiyo jana
Dk. Harrison Mwakyembe wa pili kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wabunge, kushoto ni Mbunge wa Same Mashariki Mama Anne Kilango Malecela, Waziri wa Afrika Mashariki Samwel Sitta na Mbunge wa Kahama Bw. James Lembeli.Dk Harrison Mwakyembe Mbunge wa Kyela na Naibu Waziri wa Ujenzi katika ibada iliyofanyika jana kwenye kanisa hilo na kuhudhuriwa na Waziri wa Afrika Mashariki mzee Samwel Sitta na baadhi ya wabunge kadhaa, Mzee Samwel Sitta amesema Mwakyembe amekwenda kanisani hapo ili kutoa ushuhuda kuhusu ugonjwa wake kwa ujumla. Dk. Harrison Mwakyembe ametoa ushuhuda akimshukuru mungu kwa kumbariki na kuendelea kumpa nguvu juu ya afya njema, Mwakyembe ambaye alikuwa amevalia kofia na Glovu katika mikono yake, ameongeza kwamba tangu alipokuwa ameondoka kwenda nchini India kwa matibabu Oktoba 9 mwaka jana hakuwahi kuvaa viatu, lakini leo amevaa, hivyo akamshukuru mungu kwa miujiza yake.Picha na John Bukuku

Tuesday, January 24, 2012

Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kupitia kitengo chake cha utatuzi wa migogoro (Dispute Resolution Chamber- DRC) limeagiza klabu ya Yanga kumlipa mchezaji John Njoroge sh. 17,159,800 ikiwa ni fidia kwa kuvunja mkataba wake kinyume cha taratibu.
Uamuzi huo wa DRC chini ya Jaji Theo van Seggelen ambaye ni raia wa Uholanzi ulifanywa Desemba 7 mwaka jana jijini Zurich, Uswisi na kutumwa TFF kwa njia ya DHL, Januari 17 mwaka huu.
Njoroge ambaye ni raia wa Kenya aliwasilisha kesi yake FIFA kupinga Yanga kuvunja mkataba alioingia wa kuichezea timu yao kinyume na makubaliano. Mchezaji huyo hivi sasa anachezea timu ya Tusker ambayo ni mabingwa wa Kenya.
Yanga ina siku nne za kukata rufani kupinga uamuzi huo kuanzia tarehe iliyoupokea kama inataka kufanya hivyo. Klabu hiyo inatakiwa iwe imeshamlipa Njoroge ndani ya siku 30 tangu ilipopokea uamuzi huo. Ikishindwa kulipa ndani ya muda huo, itatozwa riba ya asilimia 5 kwa mwaka ya fedha hizo.
Ikiwa Yanga itashindwa kulipa ndani ya muda huo vilevile suala hilo litafikishwa mbele ya Kamati ya Nidhamu ya FIFA kwa hatua zaidi.

Fissoo:Wasanii Zijueni Sheria Za Filamu na Michezo Ya Kuigiza



Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Joyce Fissoo akionesha Sheria namba 4 ya mwaka 1976 ya Utengenezaji wa Filamu na Michezo ya Kuigiza kwa waandishi wa habari ambao hawapo pichani wakati akitoa ufafanuzi wa kuhusu sheria hyo kwa vyombo vya vya habari leo jijini Dares Salaam.
-----
Benjamin Sawe-Maelezo Dar es Salaam
Wasanii wa Filamu na Michezo ya Kuigiza wameshauriwa kuzisoma nyaraka mbalimbali za Bodi ya Filamu ili wajue sheria na kanuni zinazohusu tasnia ya hiyo.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Joyce Fissoo alipokuwa akitoa ufafanuzi juu ya Sheria namba 4 ya Utengenezaji wa Filamu na Michezo ya Kuigiza ya mwaka 1976.

Akifafanua juu ya sheria hiyo, Bi Fissoo alisema ndiyo inayoendelea kutumika mpaka sasa na kukanusha tuhuma zilizosambazwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa ya uwepo wa matumizi ya sheria mpya.

“Hakuna Sheria mpya ya Filamu na Michezo ya Kuigiza iliyotungwa, Sheria inayoendelea kutumika ni ile ya mwaka 1976 bali kilichofanyika ni utekelezaji wa kanuni za sheria ya filamu na michezo ya kuigiza ambapo mchakato wake ulianza mwaka 2011.

Akizungumzia juu ya malalamiko ya baadhi ya wasanii kushindwa kuhimili kulipa ada ya Sh. 500,000(laki tano) Bi. Fissoo alisema kifungu cha 8 cha sheria hiyo kinampa Waziri mwenye dhamana husika kutoa msamaha wa malipo kwa msanii mchanga atakayeshindwa kulipa kiasi cha fedha hizo.

“Ada wanayolipa wasanii ya Sh.500, 000 (laki tano) ipo toka siku za nyuma ambapo Sheria namba 4 ya Filamu na Michezo ya kuigiza inampa mamlaka Waziri husika kutoa msamaha kwa msanii mchanga atakayeshindwa kulipa ada hiyo”.alifafanua.

Alisema kwamba msamaha wa ada ya sh. 500,000 utatatolewa pale tu msanii atakapotoa taarifa kwa Waziri husika na mara baada ya kujiridhisha ndipo msamaha utatolewa na kutangazwa kwenye gazeti la Serikali.

Amewashauri wasanii wa Filamu kuwa Wazalendo kwa kutengeneza filamu zenye maadili ya Mtanzania na si kutengeneza Filamu zenye maudhui ya kimagharibi.