This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Tuesday, June 26, 2012

Ratiba ya Kagame hadharani




Na Mwandishi Wetu

RATIBA ya michuano ya Kombe la Kagame inatarajiwa kutolewa Ijumaa ijayo jijini Dar es Salaam ikiwa ni maandalizi ya michuano hiyo mikubwa kwa ngazi ya klabu katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Katibu Mkuu wa Baraza la vyama vya soka Afrika Mashariki Kati, (Cecafa) Nicholas Musonye  amesema kwamba, kabla ya kutolewa kwa ratiba hiyo itafanyika droo ya kupata makundi.

Aidha katibu huyo amesema kuwa, wanachosubiri hivi sasa ni uthibitisho wa klabu ya El Merriekh ya Sudan pekee, ambayo awali ilikuwa kwenye hatihati ya kutoshiriki michuano hiyo kutokana na sababu mbalimbali.

“Tunasubiri El Merreikh ambayo inatakiwa kuthibitisha ushiriki wao kwani klabu karibu zote zimeshafanya hivyo.

“Endapo itashindwa kuthibitisha ndani ya muda unaotakiwa tutachukua hatua ya kuiweka timu nyingine badala ya El Merriekh kwani tunahitaji kuwa na mashindano yenye ushindani wa kweli mwaka huu na bora zaidi kuliko miaka mingine,” alisema Musonye raia wa Kenya.

Baadhi ya timu nyingine ambazo si kutoka ukanda wa Cecafa ambazo zinatarajiwa kujumuishwa kwenye michuano ya Kagame msimu huu ni Vita Club ya DR- Kongo, Bloemfontein Celtics, Platinum FC na Silver Stars FC zote za Afrika Kusini pamoja na Dynamos ya Zimbabwe.

Michuano mwaka huu ya Kagame inatarajiwa kuanzia kutimua vumbi Julai 14 mwaka huu huku viwanja vya Taifa na Chamazi vikitumika kwenye michuano hiyo.

Kwa Tanzania Bara timu zitakazoshiriki ni Yanga ambao ni Mabingwa wa tetezi, Simba na Azam huku Kenya ikiwa na timu ya Tusker wakati Burundi  ikiwakilishwa na Atletico.

Aidha kwa mara ya kwanza nchi ya Sudan Kusini nayo itawakilishwa na Wau Salam wakati, Zanzibar ikiwa na kikosi cha Mafunzo, Uganda ikiwalishwa na URA na APR ikishiriki kwa niaba ya Rwanda.

Timu nyingine ni pamoja na Elman ya Somalia, Ports ya Djibouti, Red Sea ya Eritrea na mabingwa wa Ethiopia Coffee. Msimu uliopita, Yanga ilifunga Simba bao 1-0 na kutwaa ubingwa katika mchezo wa fainali ulipigwa  Julai 10 mwaka jana.

Wednesday, June 20, 2012

Mayay aenguliwa uchaguzi Yanga



Kutoka ndandao wa Bin Zuber

KAMATI ya Uchaguzi ya klabu ya Yanga ya Dar es Salaam, imemuengua mgombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti, Ally Mayay Temebele kwa sababu mbili; kwanza pingamizi alilowekewa na pili kuidharau Kamati hiyo kwa kutofika kwenye usikilizwaji wa pingamizi lake bila ya taarifa yoyote.

Katibu wa Kamati hiyo, Francis Kaswahili ameambia BIN ZUBEIRY jioni hii kwamba pingamizi alilowekewa Mayay lilistahili majibu yake, lakini kwa kuwa hakutokea Kamati imeona mambo mawili, mtoa pingamizi ana hoja na pili Mayay ameidharau Kamati hiyo kwa kutofika bila taarifa.

Kaswahili alisema pingamizi dhidi ya ‘Meja’ Mayay, Nahodha wa zamani wa Yanga lilikuwa kuhusu kushindwa kutekeleza majukumu yake awali, akiwa kiongozi wa klabu hiyo na ndani ya muda mfupi anaomba tena uongozi.

“Wagombea wengine wote wamepitishwa kuendelea na usajili kwa ajili ya uchaguzi, isipokuwa Ally Mayay pekee,”alisema Kasawahili.

Kuenguliwa kwa Mayay, kunafanya nafasi ya Makamu Mwenyekiti ibakiwe na watu watatu, ambao ni Ayoub Nyenzi, Yono Kevela na Clement Sanga, wakati wagombea Uenyekiti ni Yussuf Mehboob Manj, John Jambele, Edgar Chibura na Sarah Ramadhani.

Katika nafasi za Ujumbe ni Lameck Nyambaya, Ramadhani Mzimba ‘Kampira’, Mohamed Mbaraka, Ramadhani Said, Edgar Fongo, Beda Simba, Ahmad Gao, Mussa Katabaro, George Manyama, Aaron Nyanda, Abdallah Bin Kleb, Omary Ndula, Shaaban Katwila, Jumanne Mohamed Mwammenywa, Abdallah Mbaraka, Peter Haule, Justin Baruti na Abdallah Sharia.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, Mfanyabiashara Muzamil Katunzi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eliakhim Masu walichukua fomu za kugombea Ujumbe lakini wakashindwa kurudisha, wakati Isaac Chanzi pia hakurudisha fomu ya Makamu Mwenyekiti hivyo moja kwa moja hao hawamo katika kinyang’anyiro.

Uchaguzi huo, unaokuja baada ya Wajumbe wengi wa Kamati ya Utendaji katika uongozi uliokuwa madarakani, akiwemo Mwenyekiti Wakili Lloyd Baharagu Nchunga na Makamu wake, Davis David Mosha kujiuzulu utafanyika Julai 15, mwaka huu Dar es Salaam.

Mapema jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya klabu hiyo, walipokea pingamizi dhidi ya wagombea Uenyekiti, Manji na Sarah Ramadhani, Makamu Mwenyekiti, Yono Kevella, Clement Sanga na Ally Mayay.

Lakini Jaji Mkwawa amesema Kamati yake inaweza kusikiliza na kuamua kuhusu mapingamizi hayo bila ya kuwepo waliowekewa au walioweka, ila tu amesistiza ni vema wakawepo ili watetee hoja zao.

Aidha, kuhusu tamko la mwanachama Abeid Abeid ‘Falcon’ kutaka ufafanuzi wa Katiba ipi itatumika katika uchaguzi huo, Jaji Mkwawa alisema itatumika Katiba ya mwaka 2010 iliyowasilishwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Juni 17, mwaka huo.
Amemtoa wasiwasi Abeid kwamba katiba ya 2011 iliyokuwa na matatizo kiasi cha kupingwa mahakamani na wanachama wa klabu hiyo haitatumika.

Lakini pia, Mkwawa amesema pamoja na kwamba uchaguzi huu unakuja baada ya Wajumbe wengi wa Kamati ya Utendaji, wakiwemo Mwenyekiti na Makamu wake kujiuzulu, Wajumbe waliojiuzulu kutoka kwenye uongozi huo wanaruhusiwa kugombea.
Aidha, kuhusu wagombea kusaidia klabu katika masuala yanayohusu fedha katika kipindi hiki kigumu, Jaji Mkwawa amesema hayana matatizo yakifanyika katika taratibu zinazoeleweka.

Baada ya kusikiliza pingamizi kesho, Jaji Mkwawa amesema usaili utafanyika Juni 22 na Uchaguzi wa Yanga utafanyika Julai 15 kama ilivyopangwa, siku moja baada ya kuanza kwa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, michuano ambayo, Yanga ni bingwa wake mtetezi.    

Monday, June 18, 2012

nyota Yanga atua Coasta

 
Aliyekuwa shambuliaji nyota wa kikosi cha Yanga B, Atupele Green amejiunga na klabu ya Coastal Union kwa mkataba wa miaka mitatu ikiwa  ni maandalizi ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Akizungumza na Smtandao huu, Green alisema kuwa amevutiwa na dau alilopewa na Coastal ambapo ameongeza kuwa anaimani kuwa atapata nafasi ya kucheza zaidi tofauti na klabu nyingine.

Kadhalika amefafanua kwmaba hana mpango na kucheza katika klabu za Simba wala Yanga kwani anachikiangalia kwa sasa ni kucheza soka la kulipwa.

“Nimeona kwamba hapa ndipo patakapokuw ana maisha bora ya baadaye kwenye soka langu, imani yangu ni kwmaba nitaweza kupata mafanikio makubwa katika siku zijazo hivyo sina shaka.

“Nihitaji kucheza soka kwa muda mrefu zaidi ambapo ili kufanya hivi ni lazimia kwenye  klabu ninatakayopata nafasi ya kutumika.

“Ninachikiamini ni kwamba, nataka kufanya kazi kubwa kwa ajili ya nchi hii ninaangalia namna bora ya kuweza kutangaza jina langu na nchi yangu hivyo hapa Coastal ndiyo nimeona panaweza kunifaa ndiyo maana nimekubali kuja.

“Pia nimepewa dau nililokuwa nalihitaji kwa kama nilivyokuwa nimepanga akilini mwangu,” alisema Green ambaye aliitumikia Yanga miaka mitano.

Katika hatua nyingine nyota huyo amesisitiza  kuwa baada ya mkataba wake kumalika ataangalia kucheza soka la kulipwa nje ya nchi na hatakuwa na mpango wa kucheza kwenye Ligi kuu ya Tanzania Bara.

Awali Green alikuwa asajiliwe na Yanga lakini ilitokea hali ya kutoelewana baina ya pande hizo mbili hali iliyofanya mkataba uliyokuwa umeandaliwa kwa ajili yake kuchanwa hadharani.

Sunday, June 17, 2012

MBUNGE WA SINGIDA MJINI MOHAMED DEWJI ATOA MSAADA WA PIKI PIKI JIMBONI


Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohammed Gullam Dewji akizungumza na wafanyabiashara wa bodaboda (hawapo kwenye picha) muda mfupi kabla hajawakabidhi msaada wa pikipiki kumi zenye thamani ya shilingi milioni 20.Kushoto ni katibu wa umoja wa wafanyabiashara wa bodaboda, Maulid Mpondo.Kulia wa kwanza ni Kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Singida,Williamu Haaly na anayefuata,ni katibu wa CCM manispaa ya Singida.


Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohammed Gullam Dewji akimkabidhi katibu wa umoja wa wafanyabishara wa bodaboda msaada wa pikipiki 10.
Pikipiki 10 aina ya sanlag CC150 zilizotolewa msaada ya mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mohammed Gullam Dewji kwa vikundi 10 vya wafanyabiashara wa bodaboda mjini Singida.

Baadhi ya wafanyabiashara wa bodaboda wa mjini Singida wakiserebuka na kucheza 'KIDUKU' na mbunge wao Mohammed Gullam Dewji muda mfupi kabla ya mbunge huyo kuwakabidhi wafanyabiashara hao msaada wa pikipiki.



Na Geofrey Mwakibete na Nathaniel Limu
Wafanyabiashara wa bodaboda jimbo la Singida mjini,wamehimizwa kuunda/kuanzisha vikundi ili pamoja na mambo mengine, kujijengea mazingira mazuri ya kukopesheka.
Wito huo umetolewa na mbunge wa jimbo la Singida mjini,Mohammed Gullam Dewji,wakati akizungumza kwenye hafla iliyofana, ya kukabidhi pikipiki 10 aina ya sanlag CC 150 zenye thamani ya shilingi milioni 20 kwa vikundi vya wafanyabiashara wa bodaboda.
Alisema faida za kujiunga kwenye vikundi ni nyingi ikiwemo ya kuwa nafasi nzuri ya kupata mikopo mbalimbali kutoka kwenye taasisi za kifedha.Mtu mmoja mmoja akitaka kukopa fedha benki ni ngumu, kuotokana masharti yaliyowekwa na taasisi za kifedha.
“Siku zote umoja ni nguvu,utegano unachangia kuleta ulegevu unaozaa udhaifu.Mahali pana ulegevu,kwanza hakuna maendeleo ya kweli na pia kutetea haki,inakuwa ngumu mno”,alifafanua Dewji ambaye pia ni mjumbe wa NEC CCM mkoa wa Singida.
Kuhusu pikipiki hizo alizotoa msaada, alisema lengo lake ni kwamba kila kikundi kitaitumia pikipiki yake kwa ajili ya kukiongezea kikundi mapato ambayo endapo yatatunzwa vizuri,ipo siku kila mwanakikundi anaweza akamiliki pikipiki yake binafsi.
Aidha, amewataka wakati wote kuzingatia sheria halali zilizowekwa na mamlaka husika, ili shughuli zao ziweze kuendelea bila matatizo.
“Pia napenda kutumia fursa hii, kuomba mamlaka zinazohusika na sheria za usalama barabarani na utozaji wa kodi na ushuru, kujipanga kwa ajili ya kutoa elimu kwa wafanyabiashara wa bodaboda,ili waweze kuzifahamu sheria husika”,alisema na kuongeza;
“Nina imani kwamba wafanyabiashara wa boda boda wakifahamu kwa kina sheria za usalama barabarani,kutapunguza mno ajali na pia wakifahamu mambo ya kodi na ushuru,hawatakwepa kulipa”.
Katika hatua nyingine, Dewji amewahimiza waumini wa madhehebu ya dini, kuongeza kasi ya utoaji sadaka,ili kuimarisha ustawi wa madhahebu yao.
Alisema waumini wanao wajibu mkubwa wa kuchangia kwa hali na mali madhehebu yao kwa lengo yaweze kutekeleza wajibu wake kwa ufanisi zaidi.
“Sadaka inayotolewa kwa moyo mkujufu,licha ya kusaidia ustawi wa dhehebu la dini husika,mtoaji anakuwa amejiwekea thawabu mbele ya mwenyezi Mungu”,alisema Dewji.
Akiijengea nguvu hoja yake hiyo,mbunge huyo, alisema ustawi wa kweli wa dhehebu la dini,utaletwa na waumini wenyewe,watu wengine/taasisi zingine,kazi zao ni kusaidia mahali waumini wanapokuwa wamepelea.
Katika siku yake ya pili ya ziara yake ya kikazi jimboni kwake,Dewji alitoa msaada wa mifuko ya saruji 40 kwa msikiti wa kijiji cha Manguamitogho na mifuko mingine 25 ya saruji na shilingi laki tano taslimu, kwa kanisa la Pentekoste la kijiji cha Ititi.
Katika siku yake ya mwisho ya ziara yake (17/6/2012),Dewji alitarajiwa kuwa na kikao maalum na madiwani wa kata za Singida mjini,kuzindua kisima cha maji cha kijiji cha Mtisi,kuzungumza na wanachama wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Singida na kukagua kituo cha afya cha Sokoine mjini Singida

MWILI WA MAREHEMU WILLY EDWARD UKITOLEWA WASAFIRISHWA KWENDA DAR


Kaka mkubwa wa marehemu aliyekuwa Mhariri Mkuu wa gazeti la Jambo Leo, Willy Edward
Ogunde, George Ongiri Ogunde (wa kwanza kulia) akishirikiana na ndugu, jamaa na waandishi wa habari, kubeba mwili wa mhariri huyo, aliyefariki dunia ghafla jana usiku eneo la Forest Hill, mjini Morogoro. Mwili huo ulikuwa unatolewa chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kusafirishwa kwenda jijini Dar es Salaam kwa maandalizi ya mazishi katika Kijiji cha Mugumu kilichopo wilaya ya Serengeti, mkoani, Mara.. (PICHA ZOTE NA JUMA MTANDA BLOG)
Mbunge wa Jimbo la Morogoro, Azizi Abood, akiwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006), Husein Bashe wakisubiri kuuona mwili wa Willy Edward
Baadhi ya waandishi wa habari akiwemo Mbunge wa Morogoro mjini, Azizi Abood, wakiwa na huzuni walipokuwa wakisubiri kutoa heshima za mwisho katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro, muda mfiupi kabla ya mwili kusafishwa Dar es Salaam.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Joel Bendera (kulia) akisikiliza jambo kutoka kwa kaka mkubwa wa
marehemu aliyekuwa mhariri mkuu wa gazeti la Jambo Leo, Willy Edward Ogunde, George Ongiri
Ogunde muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kwenda jijini Dar es Salaam kwa maandalizi ya mazishi katika kijiji cha cha Mgumo kilichopo wilaya ya Serengeti mkoani Musoma. wa pili kutoka kulia ni Katibu Tawala wilaya ya Morogoro, Alfred Shao na kaka mkubwa upande wa baba, Isack Ugunde.

Friday, June 15, 2012

Cholo, Mweta waendelea kula bata Msimbazi


Na Mwandishi Wetu

UONGOZI wa Klabu ya Simba umesisitiza kuwa hauna mpango wa kumtema beki wa klabu hiyo, Nassor Said ‘Cholo’ pamoja na Wilbert Mweta katika usajili ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga amesema Simba wachezaji hao hawapo kwenye orodha wa wale watakaotemwa katika usajili  wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.

“Simba ina mipango mingi lakini katika usajili wake hatutawaacha nyota hao kama ambavyo wengi wanavyoamini kwa sababu hawapo kwenye orodha ya wale wataoachwa.

“Kama kuna taarifa za majeruhi  ni suala la ndani ya Simba na si busara kuliweka wazi, ila ninachosisitiza nikiwa ni kiongozi wa Simba kwamba Cholo na Mweta wataendela kuwepo klabuni msimu ujao wa ligi.

“Pia wakati wa kuwaacha wachezaji kwa ajili ya msimu ujao bado hivyo kauli za sasa kuwa tunamuwacha fulani na fulani anabakia si taarifa kutoka ndani ya Simba ambazo tunaziona kuwa na malengo mabaya na klabu yetu.
“Tunasema si sahihi kwa sababu wapo baadhi ya wachezaji waliomaliza mkataba na Simba lakini kutokana na umuhimu wao yapo mazungumzo yanayoendelea baina ya pande mbili hizi.

“Nichukue nafasi hii kuwasihi wanachana na wapenzi wa Simba kuwa makini katika wakati huu na wasiyumbishwe bali wasubiri taarifa rasmi itatolewa na uongozi,” alisema Kamwaga.

Cholo aloijiunga na Simba akitokea JKT Oljoro ya Arusha katika usajili wa ligi kuu msimu uliopita huku, Mweta akitua akitokea Toto Africans ya jijini Mwanza. Pamoja na usajili huo, Cholo ndiye aliyepata nafasi kubwa ya kucheza zaidi ya Mweta ambaye hakupata nafasi kutokana na uwepo wa kipa namba moja Juma Kaseja.

Simba yalegezea bilioni 2 za Okwi



Ezekiel Kamwaga  msemaji wa Simba

Na Mwandishi Wetu
KLABU ya Simba imelegeza msimamo wake baada ya kusema kuwa dau la sh bilioni mbili iliyokuwa imetangaza awali kwa klabu inayotaka kumsajili mshambualiaji wake, Emmanuel Okwi kuwa linaweza kupungua au kuongezekana.
Akizungumza na tanzaniacelebrity.com msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema kuwa Simba itakuwa tayari kufanya mazungumzo juu ya dau halisi la nyota huyo ambapo dau hilo litategemea klabu inayomuita inaweza kutoa kiasi gani cha fedha.
Kwa sasa Okwi ameitwa katika majaribo nchini Afrika Kusini katika klabu ya Orlando Pirates ambapo kama akifuzu ndiyo mazungumzo ya uhamisho wake yatafanyika.
 “Tupo tayari kumwachia kwa dau tutakalokubaliana lakini kwa hivi sasa tunachoangalia ni kumsaidia kwa hali na mali ili aweze kwenda na kufuzu majaribio yake kwani itakuwa ni sehemu muhimu ya kuitangaza klabu yetu.
 “Ni kweli awali tulitangaza dau hilo lakini kwa sasa tunasubiri kwanza kama atafuzu ndiyo tutakuwa kwenye wakatiu mzuri wa kujua anasajiliwa kwa kikasi gani kwa sababu  itategemea klabu inaweza kutoa kiasi gani.
 “Kimsingi kama unavyojua katika usajili huwa kunakuwa na mambo mengi lakini imani nyetu ni kwamba Simba inaweza kumuachia Okwi kwa dau lolote kwa kuwa linaweza kuongezeka au kupungua,” alisema Kamwaga.
Awali Simba ilitangaza kumuachia Okwi kwa dau la sh bilioni mbili kwa klabu ambayo ilikuwa inahitaji kumsajili nyota huyo ambaye ameonyesha kiwango cha juu katika msimu wa uliopita.
Tayari klabu ya Orlando ya Afrika Kusini imeonekana kumhitaji mshambuliaji huyo mwepesi kwenye kikosi chake kwa ajili ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini.
Kabla ya kutua Simba, Okwi alikuwa akiitumikia klabu ya SC Villa tangu mwaka 2009 ambapo alifanikiwa kuifungia timu hiyo mabao 13 katika mechi 40 alizocheza. Hadi sasa ameipa Simba mabao 17 kati ya  mechi 27 alizocheza tangu mwaka 2010 alipojiunga na mabingwa hao wa Ligi ya Tanzania Bara.