This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Sunday, September 30, 2012

Yanga yameremeta Uwanja wa Taifa, yainyuka Lyon 3-1


Add caption

Add caption
kocha mpya wa Yanga raia wa Uholanzi, akizungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya African Lyon kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam leo. Katika mchezo mchezo wa leo Yanga ilishinda kwa mabao 3-1.

BONDIA FRANCIS CHEKA AMTWANGA KARAMA NYILAWILA KWA KO RAUNDI YA 6

BONDIA Francis Cheka jana usiku alimpiga kwa KO bondia Karama Nyilawila kwenye pambano la raundi 12 la UBO

Cheka alimpiga Nyilawila kwa KO raundi ya sita alipomtwanga ngumi iliyompeleka chini na kumfanya refa kumwesabia lakini aliponyanyuka aliamua kuvua gloves kuahashiria amekubali matokeo.

Cheka ambaye aliingia ulingoni bila mbwembwe alimwacha Nyilawila ajifurahishe kwa kurusha makonde ambayo alikuwa anayakwepa hivyo kumfanya pumzi kumwishia mapema.

Ilipotimu raundi ya tano Cheka alianza kurusha ngumi nzito nzito na kufanya ukumbi kulipuka kwa kelele za kusema " Cheka ua huyo unampotezea muda, maliza"

Bondia Karama Nyilawila akiwa amekaa ulingoni baada ya kupokea konde lililompeleka chini wakati wa pambano la UBO lililofanyika jana usiku ukumbi wa PTA sabasaba.

Bondia Francis Cheka akipangua ngumi aliyorusha Karama Nyilawila

Bondia Karama Nyilawila akiwa amemkumbatia Francis Cheka

SIMBA NOMA YAUA IKIWA PUNGUFU

Wachezaji wa Simba wakishangilia bao alilofunga Sunzu kwenye mchezo uliochezwa jana uwanja wa Taifa na Simba kushinda bao 2-1

Mshambuliaji wa Simba Felex Sunzu akiwatoka mabeki wa Prison kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa jana jioni

Baadhi ya Mashabiki wa Simba waliokuwepo uwanjani
TIMU ya Simba jana iliifunga Prison ya Mbeya bao 2-1 ikiwa pungufu baada ya beki wao Amir Maftah kuonyeshwa kadi nyekundu.

Prison ndio walikuwa wa kwanza kuliona lango la Simba dakika ya sita baada ya shuti la Lugano Mwangama kubabatiza beki wa Simba na kupoteza uelekeo hivyo kumchanganya Juma Kaseja na kutinga wavuni

Dk 44 Felex Sunzu alisawazisha bao hilo kabla ya Mrisho Ngassa kuhitimisha karamu ya mabao kuwa 2-1

Saturday, September 29, 2012

AZAM YAIENGUA SIMBA KILELENI

Golikipa wa JKT RuvuShaban Dihile akidaka mpira uliokuwa unaelekea golini mwao huku beki Hussein  Dumba akimzuia John Bocco asilete madhara
Mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara kati ya Azam na JKT Ruvu uliofanyika katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam umemalizika kwa Azam kupata ushindi wa mabao 3-0 ambapo mabao ya washindi yakiwekwa nyanvuni na John Bocco akifunga bao la kwanza kwa njia ya mkwaju wa penati na mabao mengine mawili yakiwekwa nyavuni na mshambiliaji Pipre Tcheche.
Kwa matokeo hayo Azam imefikisha jumla ya points 10 na kukalia usukani wa ligi hiyo ikifuatiwa na bingwa mtetezi Simba wenye points 9 na Coastal ikiwa katika nafasi ya tatu baada ya kukusanya jumla ya points 7.
Changamoto kubwa iliyojitokeza ni licha ya mchezo huo uliochezwa usiku na kupata nafasi ya kuonyeshwa moja kwa moja na kituo cha television cha Supersport, lakini mpira mbovu na mashabiki wachache wamefanya mchezo huo  kuonekana kutostahili kupata nafasi onyesho moja kwa moja kwani uwanja ulionekana kwenye kichupa ukiwa mweupe kiasi mpiga picha kupata wakati mgumu kuchukua sehemu ya watazamaji.
Hata hivyo lawama kwa mara nyingine zimeelekezwa kwa shirikisho la soka nchini kwa kuweka kiingilio cha juu cha shilingi 5,000 na 10,000 katika mchezo ambao timu zake hazina mashabiki wengi kama ilivyo vilabu vya Simba na Yanga.
Ligi hiyo inaendelea tena leo tarehe 29/09/2012 ambapo Simba itakuwa mwenyeji wa maafande wa Tanzania Prisons uwanja wa Taifa mchezo ambao utaanza saa 11jioni na kesho  tarehe 30/09/2012 Yanga ataikaribisha Coastal Union ya Tanga katika uwanja huo huo na kuonyeshwa live kama ilivyokuwa mechi ya leo.

KAMISAA WA SIMBA AUMIA, TFF YAMUENGUA LIGI KUU KWA KUWASILISHA RIPOTI YA POTOFU YA MCHEZO



Na Mahmoud Zubeiry
KAMATI ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ilikutana jana (Septemba 25 mwaka huu) kupitia ripoti za mechi 21 za Ligi Kuu ya Vodacom ambazo zimeshachezwa mpaka sasa, na kumuondoa George Komba aliyekuwa Kamisaa kwenye mechi namba 20 kati ya Simba na Ruvu Shooting, upungufu uliojitokeza katika ripoti yake.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace Wambura Mgoyo ameiambia BIN ZUBEIRY mchana huu kwamba, klabu ambazo zimeandikwa barua za onyo ni African Lyon kwa kwenda uwanjani na jezi tofauti na zile ilizoonesha kwenye mkutano wa maandalizi ya mechi (pre match meeting), Mtibwa Sugar kwa kuchelewa kuwasilisha leseni za wachezaji wake wakati wa mechi na Ruvu Shooting kwa ushangiliaji uliopita kiasi kwenye mechi yao dhidi ya Simba.
Amesema Kamati pia imethibitisha kadi nyekundu ya Emmanuel Okwi kwa kumpiga kiwiko Kessy Mapande wa JKT Ruvu, hivyo kwa mujibu wa Kanuni ya 25(1) anakosa mechi tatu na kulipa faini ya sh. 500,000. Mchezaji huyo atakosa mechi namba 20, 27 na 80.
Amesema kwa upande wa waamuzi, Ronald Swai ameandikiwa barua ya onyo kutokana na upungufu alioonesha kwenye mechi kati ya Simba na Ruvu Shooting iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Amesema wamiliki wa viwanja vya Mkwakwani, Tanga na Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya wameandikiwa barua ya kuvifanyia marekebisho viwanja vyao katika maeneo mbalimbali yenye upungufu ikiwemo uzio wa kutenganisha wachezaji na washabiki.
Aidha, Wambura amesema beki Faustine Lukoo wa Polisi Moro ambaye kwa mujibu wa ripoti ya mwamuzi aliyemtoa nje kwa kadi nyekundu alimtukana mchezaji mwenzake kwenye mechi dhidi ya African Lyon na Katibu wa Oljoro JKT aliyemwaga maji kwenye chumba cha timu ya Polisi Moro, masuala yao ni ya kinidhamu, hivyo yamepelekwa Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi kwa ajili ya hatua zaidi.
Amesema klabu ambazo timu zao mpaka sasa zinacheza mechi bila kuwa na logo ya mdhamini, suala hilo limepelekwa kwa wadhamini Vodacom kwa vile wenyewe ndiyo wanaogawa vifaa hivyo.
Wakati huo huo: Rais wa TFF, Leodegar Tenga atakutana na waandishi wa habari kesho mchana, kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF.
Katika hatua nyingine, Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliyokutana jana kusikiliza rufaa ya Mussa H. Mahundi, Abou O. Sillia na Alex Mgongolwa dhidi ya Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Soka Iringa (IRFA), iliyoomba Kamati ya Uchaguzi ya TFF kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa IRFA uliofanyika Septemba 8 mwaka huu Mufindi, Iringa, na kuomba uchaguzi huo ufanyike upya kwa kuendeshwa na kusimamiwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF, imetupilia mbali rufaa hiyo.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Deogratias Lyatto, baada ya kupitia maelezo ya warufani na warufaniwa, Kamati ya Uchaguzi ya TFF imejiridhisha kuwa rufani iliyowasilishwa mbele yake na Mahundi, Sillia na Mgongolwa ilikosa sifa ya kuwa rufani kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF, Ibara ya 8(2), Ibara ya 21(3) na 24(2). Kwa kutozingatia matakwa ya Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF, Kamati ya Uchaguzi ya TFF imetupa rufani hiyo.
Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeiagiza Kamati ya Uchaguzi ya IRFA kuchukua hatua dhidi ya Abuu Changawa kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF, Ibara ya 28(6) kwa kuingilia mchakato wa uchaguzi wa IRFA siku ya uchaguzi.

HIVI NDIVYO AGNES YAMO ALIVYOAGWA LEO, NI VILIO HADI KUZIRAI

Mwili wa aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa gazeti la Tanzania Daima, Agness Christopher Yamo umeagwa leo mchana Buguruni, Dar es Salaam, tayari kwa safari ya mazishi kesho mjini Morogoro. Yamo aliyewahi pia kufanya New Habari 2006 Limited, alifariki dunia jana katika hospitali ya Jeshi, Lugalo, Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa kwa matibabu.
Katika uagwaji wa mwili wa marehemu, aliyekuwa mcheshi na rafiki wa wengi, mamia walijitokeza na wengi walishindwa kujizuia kiasi cha kulia hadi kupoteza fahamu. Hakika ilikuwa huzuni, simanzi na majonzi eneo la tukio. Agness ameliza watu. Mungu aiweke pema peponi roho ya marehemu, Amin.  
Waombolezaji

Waombolezaji











































Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda 

Mkurugenzi wa Tanzania Daima, Lillian Mbowe