This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Tuesday, November 27, 2012

Dk Ali Shein katika ziara Vietnam



 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa tatu kulia) akiwa na ujumbe wake wakipata maelezo walipotembela katika mabwawa ya ufugaji wa Samaki katika Chuo cha Uvuvi wa Samaki na ufugaji katika jimbo la Quang Ninh Mjini Halong nchini Vietnam,akiwa katika Ziara ya kiserikali
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipowasili katika Chuo cha Uvuvi wa Samaki ikiwemo na ufugaji katika jimbo la Quang Ninh Mjini Halong nchini Vietnam,akiwa katika Ziara ya kiserikali.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,na ujumbe wake wakiwa na mazungumzo na Do Quang Sang,(kulia) Mkurugenzi pia Mwenyekiti wa Kampuni ya Bidhaa za Baharini,wakiwemo Samaki,Kamba pia usindikaji katika jimbo la Quang Ninh Mjini Halong nchini Vietnam,akiwa katika Ziara ya kiserikali
 Baadhi ya Viongozi wa Chuo cha Uvuvi wa Samaki ikiwemo na ufugaji katika jimbo la Quang Ninh Mjini Halong nchini Vietnam,wakiwa katika mkutano na ujumbe wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,ukiongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,katika ziara maalum ya Kiserikali nchini humo.
Balozi wa Tanzania nchini China ambae anawakilisha Vietnam Philip Sang’ka Marmo,(kutoka kushoto) Waziri wa Kilimo na Maliasili Suleiman Othman Nyanga,na Mshauri wa Rais Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Mohamed Ramia,wakiwa katika Mkutano na Uongozi wa Chuo cha Uvuvi wa Samaki na Ufugaji katika Jimbo la Quang Ninh Mjini Halong nchini Vietnam
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(kulia) akiangalia Samaki na Kamba waliokiwisha sindikwa ikiwa ni tayari kwa usafirishaji, alipotembelea katika kiwanda cha (Quang Ninh Sea Products Import Export Company) katika jimbo la Quang Ninh Mjini Halong nchini Vietnam,alipokuwa katika ziara ya Kiserikali,(kushoto) Mkurugenzi pia Mwenyekiti wa Kampuni kampuni hiyo, Do Quang Sang,(katikati) Nguyen Ha Dieu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiagana na Do Quang Sang,Mwenyekiti pia Mkurugenzi wa Kampuni ya Import Export inayosindika na Bidhaa za Baharini katika Jimbo la Quang Ninh Mjini Halong Nchini Vietnam,baada ya kutembelea Kampuni hiyo,akiwa katika ziara ya Kiserikali.Picha na Ramadhan Othman,Ikulu-Zanzibar.

Chipukizi watesa Wazalendo awards 2012




KINYANG’ANYIRO cha kumpata mwanasoka bora wa mwaka 2012 katika tuzo za kila mwaka za Wazalendo, kimefikia pazuri baada ya majina ya wachezaji wachanga kuonekana kujitokeza zaidi ikilinganishwa na wale wenye umri mkubwa.

Mratibu wa tuzo hizo, Ahadi Kakore alisema kuwa tuzo za mwaka huu zimeonakana kuwa na msisimko mkubwa ambapo majina ya wachezaji wenye umri mdogo ndoyo yaliyopendekezwa zaidi ikilinganishwa na wakongwe.

“Tunafahamu kwamba kamati inaendelea na kazi yake ya kupembua majina lakini jambo kubwa lilionekana ni uwepo wa wachezaji wengi wachanga ikilinganishwa na wakongwe kitu ambacho kimeonekana kuwa ni cha tofauti.

“Ukiangalia uwiano yawachezaji wachanga na wakongwe ni dhahiri utaona kwamba kazi iliyopo  mbele ni kubwa katika kuhakikisha kuwa mambo yanakwenda sawa.

“Tunaimani kwamba angalau hadi kufikia tarehe za mwanzo za mwezi Desemba, tunaweza kujua mwelekeo kuwa nani ameingia na nani ameshindwa kuingia katika fainali.

“Kadhalika niwapongeze wote ambao wameendelea kutuunga mkono kwenye jambo hili kubwa katika maendeleo ya soka la Tanzania,” alisema Kakore.

Tunzo za Wazalendo zinatarajiwa kufanyika Desemba 30 mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo mshindi atapata tuzo, medali, cheti pamoja na fedha taslim.

R.I.P Sharo Milionea



Marehemu Sharomilionea enzi za uhai wake

Taarifa kuhusu kifo cha Msanii wa maigizo na Mziki wa Bongo fleva kufariki zimasamba nchi nzima masaa machache yaliopita.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari ni kwamba amepata uthibitisho kutoka kwa diwani Makame Seif ambaye ni rafiki yake wa karibu sana wa Marehemu Hussen Ramadhani Mkiete maarufu kama Sharo Millionea amepata ajali mida ya saa mbili eneo la maguzoni Tanga na amefariki dunia papo hapo.

Polisi walitambua ni Sharo Millionea kwa vitambulisho vyake na picha moja ya passport aliokuwa nayo mfukoni ambavyo kwa sasa viko na polisi.
Diwani huyu alimfahamisha mwandishi kuwa Sharo Millionea aliumia vibaya sana kichwani, kifuani na kwenye mikono.
Pia Mjomba wa marehemu amethibitisha kuwa Sharo Millionea atazikwa Tanga na asubuhi ya leo ratiba ya msiba ingetolewa.
Ndugu na marafiki wa Sharo wameanza kwenda hospitalini baada tu ya taarifa hizi kuwafikia. Familia ya Sharo iliwasiliHospitali ya Teule ya Tanga mara baada ya kupata taarifa hizo.

 
Hii ndiyo gari aina Toyota Harrier yenye namba T278 BVR iliyopinduka na kusababisha ajali iliyopelekea kifo cha msanii Sharo milionea jana usiku mishale ya saa mbili.

Tuesday, November 20, 2012







HATUA ya utoaji wa tuzo za mwanasoka bora wa mwaka 2012, (Wazalendo Footballer of the Year)  imefikia patamu ambapo sasa fainali itafanyika Desemba 30 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mratibu wa tuzo hizo, Ahadi Kakore  amesema kuwa tuzo za Wazalendo zitakua za tofauti lakini zikiwa na lengo la kusaidia maendeleo ya soka lakini pia suala la uchumi kwa wachezaji husika.

“Hadi sasa majina 93 yameshapigiwa kura na wadau wa soka ambapo kamati inahitaji majina 30 tu hivyo katika hatua hii vipio vigezo ambavyo vinaangaliwa kwa makini kabla ya kufanyika maamuzi ingawa mchakato wa kupitia majina unaendelea. 

“Pia utoaji huu wa tuzo utakwenda sambamba na kutoa elimu ya uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali ya maendeleo ili kuongeza kipato cha wachezaji wetu ambaho kinaweza kuwasaidia hata baada ya kustaafu soka. Semina hiyo itafanyika Desemba 19 na 20 mwaka huu.

“Katika suala la afya, kamati itatumkia siku hizo mbili za semina ya uwekezaji kutoa elimu ya afya kwa wachezaji kwani afya ni jambo la kwanza kwenye michezo na uhai wa mwanadamu.

“Sababu ya kufanya semina hiyo  kwa wachezaji ni katika kuhakikisha kwamba  wachezaji wanapata maisha bora kwani wengi wa wachezaji wetu ni masikini jambo ambalo linawafanya kuendelea na hali hiyo hata baada ya kustaafu soka na baadhi yao kujikuta wanakuwa ombaomba wakati walifanya kazi kubwa kwa ajili ya nchi jambo ambalo si sahihi,” alisema Kakore.

Katika hatua nyiongine, Kakore alisema kuwa mshindi wa tuzo hiyo atapata tuzo, fedha taslim, medali na cheti. Licha ya kuwepo kwa tuzo hiyo ya mwanasoka bora lakini zitakuwepo nyingine tisa tofauti.