This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Friday, February 22, 2013

WADAU WA PSPF WAONESHWA NYUMBA ZA MKOPO ZILIZOPO BUYUNI CHANIKA

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Adam Mayingu akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara ya viongozi wa Manispaa ya Ilala pamoja na wadau wa mfuko huo walipotembelea mradi wa nyumba za ambazo zitakopeshwa kwa wanachama wake zilizopo Buyuni, Chanika nje kidogo ya Dar es Salaam jana. (Picha na Dande JR)

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Adam Mayingu (wa tatu kulia) wakati wa ziara ya viongozi wa Manispaa ya Ilala pamoja na wadau wa mfuko huo walipotembelea mradi wa nyumba za PSPF zilizopo Buyuni, Chanika nje kidogo ya Dar es Salaam

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Adam Mayingu (katikati) akiwaonesha maofisa wa Jeshi la Polisi moja ya nyumba 491 zilizopo katika mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu ambazo zitakopeshwa kwa wanachgama wa mfuko huo.


ILALA, Dar es Salaam

Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) umekamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa nyumba 641 katika mikoa mitano ambazo zilianza kuuzwa tangu Novemba mwaka 2012. Mradi huo unalenga kutatua tatizo la makazi kwa wanachama wake na jamii kwa ujumla.

Mikoa iliyojengwa nyumba hizo na idadi ya nyumba katika mabano ni Dar es salaam – Buyuni (491), Morogoro – Lukobe (25), Shinyanga – Ibadakuli (50), Tabora – Usule (25) na Mkoa wa Mtwara – Mang’amba (50).

Aidha kwa Muji wa maelezo ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bwana Adam Mayingu amewaambia wanaadishi wa habari na viongozi mbalimbali waliotembelea eneo la mradi huo Mkoawa Dar es Salaam kuwa Shirika lake limejenga nyumba za aina nne ambazo ni za nyumba viwili, Vyumba vitatu, Nyumba za vyumba vitatu kimoja ikiwa ni Master na Nyumba ya vymba vine kimoja kikiwa ni Master.

Gharama ya ununuzu wa nyumba hizo ambazo zinauzwa kwa wanachama wa Mfuko huo ni kati ya Shilingi Milioni 64 hadi milioni 94 gharama zikijumlishwa na Kodi ya ongezejo la Thamani.
 
picha na habari kwa hisani ya mtandao wa francisdande.blogspot.com

Tuesday, February 12, 2013

UCHAGUZI MKUU WA TFF HATIHATI

Na Dina Ismail
 
WANACHAMA na  mashabiki wa soka nchini wameapa kuandamana na kwenda Mahakamani kuzuia kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), baada ya Kamati ya Rufaa ya Shirikisho hilo kumuengua mgombea wa nafasi ya urais, Jamal Emil Malinzi.
 
Aidha, wanachama hao kutoka klabu za Simba, Yanga na Azam wamemtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete kuingilia kati suala la kuenguliwa kwa Malinzi kwani limefanywa kwa chuki binafsi likiwa na lengo la kumbemba mpinzani wake, Athumani Jumanne Nyamlani.
 
Wakizungumza na Waandishi wa habari leo, pamoja na kupinga kuondolewa kwa Malinzi, wametoa siku tatu kwa TFF kumrejesha katika kinyang’anyiro hicho, kinyume na hapo watakwenda kudai haki yao Mahakamani.
 
Mmoja ya wadau hao Kaisi Edwin alisema kwamba kanuni za Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) chombo cha mwisho cha maamuzi ni Mahakama yas Usuluhishi wa Migogoro ya Michezo (CAS) lakini TFF haijaelekeza baada ya kamati ya Rufaa chombo kipi kinaweza kutoa suluhu ya masuala kama hayo.
 
Alisema walitaka kupata changamoto mpya ya uongozi kupitia kwa Malinzi lakiini kitendo cha kumuengua kunaonesha ni jinsi gani wanavyotaka kuendelea kuwa na watu wasiotaka maendeleo ya soka.
 
“Ni bora tufungiwe na FIFA, tunajua maslahi wanayoyapata TFF na tutatoa uozo wote...kwa hili hata damu itamwagika na kwa gharama yoyote tutahakikisha uchaguzi haufanyiki kama wasipomrejesha Malinzi labda waende kufanyia Geneva,”aliusema Kaisi.
 
Naye Suleiman Kato alisema anashangazwa na kamati ya Rufaa kumuengua Malinzi kwa madai ya kutokuwa na uzoezfu wakati alipitishwa kugombea uchaguzi wa mwaka 2008 inagawa alishindwa kwa kura chache na rais wa sasa wa TFF, Leodger Tenga.
 
 “Malinzi pia nia mwenyekiti wa chama cha soka Kagera sasa iweje apitishe kugombea huko na mpaka anapata kiti hicho nah ii leo mseme hana uzoefu na uongozi wa soka, kinachoonekana hapa ni kutaka kudidimiza soka la Tanzania, hilo hatulikubali,”alisema.
 
Mdau mwingine, Mgeni Ramadhan ‘Dogo Macho’ alisema inaonesha wazi wazi wanataka viongozi kwa ajili ya maslahi binafsi kitu ambacho si sahihi kwani Watanzania wanaopenda soka wanataka maendeleo na si viongozi maslahi.
 
“Naamini Rais Kikwete ambaye ni mpenda michezo atasikia kilio hiki na kuingilia kati, kuna watu wapo kwa ajili ya kubebwa, huyo Nyamlani anatoka Kusini, kuna mwanakamati mmoja Murtaza mangungu ambaye ni Mbunge anambeba, pia kuna mwingine aliwahi kuwa Hakimu wa Temeke na nyamlani akiwa karani wake,”alisema.
 
Kwa upande wake, mdau mwingine Said Bakari alisema kuwa wataanza kuonesha hasira zao kuanzia leo kwenye uwanja wa Taifa kwenye mechi baina ya Yanga na African Lyon, kabla ya kuendelea na hatua yao katika michezo ya kimataifa ya timu za Simba na Azam wikiendi hii.
 
“Huyu Nyamlani anabebwa, kwani tunajua Mwenyekiti wa Kamati alikuwa rafiki yake wakati akiwa Hakimu Temeke yeye, alikuwa karani, Mangungu naye pamoja na kumpigia debe ni jirani na baba yake Nyamlani,”alisema.
 
Wadau hao kwa pamoja wamepaza sauti hizo baada kamati ya Rufaa ya TFF kumuengua Malinzi katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Februari 24 mwaka huu ambapo kwa mujibu wa ratiba kampeni zinatarajiwa kuanza leo.
Katika hatua nyingine, Malinzi kesho anatarajiwa kuzungunmza na waandishi wa habari kuhusina na sakata hilo.

Habari hii ni kwa mujibu wa mtandao wa Bin zuberi.

Saturday, January 26, 2013

HALI TETE MTWARA: AMANI IMETOWEKA, SERIKALI LAWAMANI


Update:
Nyumba ya Mkuchika inawaka moto-Newala

Taarifa za redio mbao sasa  ni kwamba wananchi wanaendelea kufanya uharibifu mkubwa huko ambapo naambiwa wamevamia gereza wakafungulia wafungwa na kisha kupiga moto gereza. Polisi wamezidiwa na wamejifungia kituoni wanarusha mabomu yao tokea huko walikojificha maana nje hakutamaniki. Na wameshateketeza nyumba ya mama Anna Abdallah.

Update:
Kikao cha dharura cha kamati ya ulinzi na usalama kinaendelea kwa kuwashirikisha maafisa wa polisi na maafisa usalama waliotoka Dar es Salaam kuongezea nguvu.

Maaskari na makachero wawasili  Mtwara leo asubuhi na helkopta kuongezea nguvu.

Hosteli ya wanafunzi wa chuo cha Utumishi maeneo ya Kiyangu B Mtwara yakoswa koswa kuchomwa moto kwa kile kinachodhaniwa kuwa na uhusiano na Hawa Ghasia mpaka sasa wanafunzi hawana mahala pa kukaa.  Kituo kidogo cha Polisi Cha Shangani mkoani Mtwara nacho chakoswa na moto. Ofisi ya Afisa Mtendaji Nkanaledi mkoani Mtwara nayo yavunjwa.

Wananchi wamechoma moto mahakama ya Mwanzo na kuvunja vioo vya nyumba za waheshimiwa Hawa Ghasia (Waziri, TAMISEMI) na ya Mohamed Sinani (Mwenyekiti wa CCM Mkoa) zilizopo mtaa wa Sinani.


Wakiwa katika mahakama ya mwanzo, Polisi walizingirwa na vijana waliokuwa wamebeba mawe na kufunga barabara zote za kuingia na kutoka Kituo Kikuu cha Mabasi na eneo la Soko Kuu, licha ya kufyatua hewani mabomu ya machozi.

Baadhi ya barabara za zimezibwa kwa kuchomwa matairi ya gari, na kuongeza hofu kwa wananchi.

Hali imeshakuwa mbaya masasi taarifa zilizotufikia punde wamechoma eneo linaloitwa loliondo, ofisi za elimu na ofisi ya trafiki, inasemekana jamaa wameshavamia ofisi za halmashauri wengine wako njiani nyumbani kwa mama Ana Abdala, hapa Mtwara  mjini maduka yote eneo la soko kuu na stendi yamefungwa hakuna huduma, huko Newala , leo kuna mkutano mkubwa mchana huu wa kumkataa George Mkuchika.

Vurugu zahamia wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Nyumba ya Mbunge wa Masasi nayo yateketezwa kwa Moto hivi sasa...Madereva Bodaboda waandamana ...Vurugu zashamiri Mabomu Kibao..Hali ni tete


POLISI jana  wamelazimika kupiga mabomu ya machozi kutwa nzima katika kata ya Chikongola, Manispaa ya Mtwara Mikindani kutawanya wananchi walioizingira nyumba ya diwani wa kata hiyo Mohamedi Chehako kwa madai ya kuwahifadhi wachawi ndani ya nyumba yake, huku mwandishi wa habari mmoja akiripotiwa kujeruhiwa.


Habari ambazo hazijathibitishwa na kamanda wa polisi mkoani hapa, Maria Nzuki zinadai kuwa majira ya saa 10 kasoro za jioni watu wanaodaiwa kuwa ni wanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) waliingilia kati na kuanza kutembeza mkong’oto kwa wananchi ili kuzima vuguvugu hilo.

Mwandishi wa habari hizi alipojaribu kuwasiliana na kamanda Nzuki kwa njia ya simu za mkononi hakuweza kupatikana.

Wananchi walitoa tuhuma hizo baada ya kukuta ungo ikiwa na tunguri ndani yake ambayo inadaiwa kuwa ni ndege ya wachawi uwanjani kwake maeneo ya makaburi Msafa.

Wananchi walijikusanya nyumbani kwa Diwani huyo na kumshinikiza awatoe wachawi nje ili waweze kuwadhibu, amri iliyopingwa na Diwani huyo. Kadiri mda ulivyokwenda ndivyo wananchi walivyozidi kuongezeka na hatimaye kulijitokeza kundi la watu walioanza kutia vurugu, hali iliyomlazimu Chehako kuomba msaada wa polisi.

Mashuhuda wa tukio walimweleza mwandishi wa habari hizi kuwa polisi walipofika waliwasihi wananchi kutawanyika kwa kuwa ungo na tunguri zake zilikuwa zimeteketezwa kwa moto na diwani huyo mbele ya wananchi hao.

Chehako akihojiwa nyumbani kwake alisema: “Wananchi waliendelea kupinga na kudai ndani ya nyumba kuna rubani na abiria wa ndege nimewahifadhi…polisi wakawachagua wananchi watano na kuingia ndani ya nyumba kuwasaka watu hao…hawakuona kitu, walitoka nje na kuwamabia wenzao hata hivyo wenzao walibisha.

Walianza kurusha mawe nyumba… polisi walianza kupambana nao kwa kuwarushia mabomu…hata hivyo wananchi walikuwa wanakimbia na kwenda upande wapili kufanya vurugu.”

Chehako alibainisha kuwa ni kawada yake kuamka alfajiri kwa ajili ya sala ya asubuhi, lakini asubuhi ya jana alishindwa kuamka mapema, hata hivyo hakuweza kuhisi jambo lolote: “Ilipofika saa 12 asubuhi nikaanza kusikia watu wakishangaa kitu nje, nilipotoka nikakuta nyungo na tunguri ndani yake…mara wakaja vijana wawili na pikipiki wakachukua ule ungo na kukimbia nao…nikawatuma vijana wawafuate waurudishe…walifanikiwa na nyungo ile ilirejeshwa nyumbani hapa na ndipo nilipouteketeza kwa moto.

Nilidhani yatakuwa yameisha, lakini wananchi waliendelea kudai nimewafungia wahuska ndani, si kweli hakuna mtu humu ndani wala mimi sijui kilichotokea hadi hivyo vitu vikawa humu ndani.”

Katika mapambano hayo ya wananchi na polisi, wananchi kwa kutumia mawe wamemjeruhi Mwandishi wa Habari wa Channel Ten mkoani hapa, John Kasembe kwa jiwe kichwani, sehemu za kisogoni ambapo ametibiwa zahanati ya Fajima na anaendelea vizuri.

Kwa mujibu wa Kasembe, alipigwa mawe kichwani akiwa kazini kukusanya habari na wananchi waliokuwa wakiwarushia mawe polisi.

Ofisa wa polisi ambaye jina lake hakutaka litajwe kwa sababu si msemaji wa jeshi hilo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa gari moja ya polisi PT 1421 limevunjwa kioo cha mbele kwa mawe.

Hadi saa 10.00 jioni bado polisi walikuwa wanaendelea kupiga mabomu ya machozi hewani huku wananchi wakionekana kujipanga katika makundi hali iliyotishia usalama wa maeneo hayo.

Hii ni kwa mujibu wa www.mtwarakwetu.blogspot.com

Friday, January 25, 2013

mambo ya tuzo safi

Maandalizi ya tuzo za wazalendo 2012 yanaendelea vizuri ambapo kila kitu kinakwenda sawa.