Tuesday, December 25, 2012

Tuzo za Wazalendo Januari 31



TUZO za Wazalendo 2012, zinatarajiwa kufanyika Januari 31 mwaka 2013 jijini Dar es Salaam badala ya Desemba 30 mwaka huu kama ilivyotangazwa hapo awali.

Mratibu wa tuzo hizo, Ahadi Kakore alisema kuwa kwamba sababu za kusogezwa mbele kwa fainali hizo ni kutoka Desemba 30 hadi Januari 31 ni kutokana na baadhi ya mambo kutokamilika kwa wakati, ingawa bado zitafanyika ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Aidha sababu nyingine ni kwamba wanakamati wengi wamekuwa kwenye pilikapilika za uchaguzi wa Chama cha Makocha Tanzania (Tafca) kwa sababu wengi wao ni wanachama hivyo jambo ambalo limesababisha kushindwa kutekeleza baadhi ya mipango yao kwa wakati.

“Zipo sababu nyingi lakini kubwa ni kwamba baadhi ya wageni muhimu ambao walialikwa asilimia (80%) wameonyesha kutokuwepo kwa tarehe hiyo kwa sababu watakuwa nje ya jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya siku kuu za mwisho wa mwaka.

“Kwa kuzingatia uzito wa jambo lenyewe kamati imeona ni busara kusogeza mbele kwa siku 30 kwa lengo la kuwapa nafasi wahusika kwa pande zote mbili kuendelea na matayarisho hayo,” alisema Kakore.

Katika hatua nyingine, majina ya wanasoka walioingia fainali ya tuzo za mwakasoka bora wa mwaka yanatarajiwa kuwekwa wazi Januari mosi mwaka huu baada ya kukamilishwa kwa mchakato wa kupitia majina 93 yaliyokuwa yamependekezwa na wadau wa soka.

Mchakato wa kumpata mwanasoka bora wa mwaka ulianza tangu Agosti mosi mwaka huu ambapo wadau mbalimbali wa ndani ya nje ya Tanzania walipendekeza majina ya wachezaji ambao walistahili kutwaa tuzo hiyo.


Tuzo za Wzalendo zinalenga katika kuinua na kutambua mchango wa maendeleo ya soka la Tanzania kwa kipindi cha mwaka wa 2012 ambapo zitakuwa zikifanyika kila mwaka lengo likiwa ni kuendeleza na kuthamini kazi ambazo zimefanywa na wanasoka na wadau wa soka kwa muda wa mwaka mmoja.

0 comments: