This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Wednesday, December 26, 2012

Yaliyojiri X-MASS


Kikosi kazi cha SKYLIGHT Bendi kikiongozwa na Joniko Flower kuporomosha burudani mwishoni mwa juma katika kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar es Salaam. USIKOSE Mkesha wa X-MASS na SKYLIGHT BAND leo Usiku kuanzia saa tatu pale pale Thai Village.
Diva's wa SKYLIGHT Band Aneth Kushaba AK 47 sambamba na Mary Lucos wakishambulia jukwaa.
SONY MASAMBA sambamba na Aneth Kushaba AK47 wakipiga shoo ya nguvu.
Muziki umenoga mpaka wengine waliamua kuvua mashati.
Pichani juu na chini ni Binti wa Kiafrika mrembo aliyeumbika kisawa sawa.... akimwaga radhi mbele ya kadamnasi kuonyesha umahiri wake wa kuzungusha nyonga wakati nyimbo ya Carolina ikiimbwa na kuwaacha hoi wengine wote waliokuwa kwenye dancing floor.
Sebene limekolea....asiyekuwa na mwana aeleke jiwe.
It's Reggae and Ragga time....Aneth Kushana AK 47 akionyesha ufundi wake.
Uzao wa BSS Mary Lucos akielekea kwenye viti kunyanyua mashabiki wake.
Mashabiki wa SKYLIGHT Band wakijimwaga kwa dancing floor.
Pichani Juu na Chini Umati wa Mashabiki wa SKYLIGHT Band wakizungusha mduara wa mbele aende mbele na wa nyuma arudi nyuma.
Pichani Juu na Chini ni Papa Justin Ndege na mdau wakiwatunza wapiga vyombo na waimbaji wa SKYLIGHT Bendi baada ya kuguswa na uimbaji pamoja na upigaji wa vyombo.
Mario Mpingirwa akionyesha jinsi gani anavyopenda kinywaji chake.
Papa Justine Ndege ( wa pili kulia) akiwa na marafiki wa karibu na mashabiki wa SKYLIGHT Bendi.
Wadau wa Makumbusho Kijitonyama, Yusuph (kushoto) huku Eric Ndalu akiwa na mai waifu.
Mdau Lussa ( wa pili kulia) alitia timu SKYLIGHT Band kula bata na marafiki zake.
One and Only Mekydiva Mash Macha (katikati) akishow love na Blogger King Kif, huku Jacqueline Mzindakaya akiipa mgongo Camera yetu.
Mdau Mwika (wa kwanza kulia) bila kukosa akishow love na marafiki zake.
Mashabiki nambari One wa Skylight Band wakishow love.
Models wakitega pozi kwa Kodak. Looking Fly Girls.
Hata shida na mtu kwa raha zake...Kuna msemo unasema 'raha jipe mwenyewe'.
King Kif na Mdau Godwin Gondwe a.k.a Double G alipita pande hizi kuchungulia burudani ya Sky Light Bendi ikoje.
Diva's wa SKYLIGHT Band Aneth Kushaba AK47 na Mary Lucos baada ya kupiga show ya nguvu walipata Ukodak.

Tuesday, December 25, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZURU KABURI LA HAYATI IDRIS ABDULWAKIL, MAKUNDUCHI, AMTEMEBELEA MZEE ALI KHAMIS ABDALLAH MUASISI WA AFRO SHIRAZ PARTY

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa pili kulia) akiwa mbele ya Kaburi la Rais wa zamani wa Zanzibar  Hayati Idris Abdulwakil, wakati alipozuru Kijiji cha Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja juzi. Rais  Wakil alifariki dunia mwaka 2001. Dk Bilal alifika  eneo hilo  juzi katika ziara yake ya kuwatembelea  wazee mbali mbali mkoani humo, jana.  (Desemba 24, 2012.
 Makamu akiondoka katika kijiji hicho cha Makunduchi baada ya kuzulu Kaburi la Hayati, Abdulwakil, jana.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mzee Ali Khamis Abdallah (98) ambaye ni mmoja kati waasisi  10,  waliokaa pamoja na  kuunganisha vyama vya African Association na Shiraz Association na kuwa Chama cha Afro Shiraz Party (ASP), wakati akiwa katika ziara yake ya kutembelea wazee, leo nyumbani kwake Mbweni, mjini Unguja. Kulia ni mke wa Mzee Ali, Asha Ali Ghulam Hussein. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mzee Ali Khamis Abdallah (98) ambaye ni mmoja kati waasisi  10,  waliokaa pamoja na  kuunganisha vyama vya African Association na Shiraz Association na kuwa Chama cha Afro Shiraz Party (ASP), wakati akiwa katika ziara yake ya kutembelea wazee, leo nyumbani kwake Mbweni, mjini Unguja.

Tuzo za Wazalendo Januari 31



TUZO za Wazalendo 2012, zinatarajiwa kufanyika Januari 31 mwaka 2013 jijini Dar es Salaam badala ya Desemba 30 mwaka huu kama ilivyotangazwa hapo awali.

Mratibu wa tuzo hizo, Ahadi Kakore alisema kuwa kwamba sababu za kusogezwa mbele kwa fainali hizo ni kutoka Desemba 30 hadi Januari 31 ni kutokana na baadhi ya mambo kutokamilika kwa wakati, ingawa bado zitafanyika ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Aidha sababu nyingine ni kwamba wanakamati wengi wamekuwa kwenye pilikapilika za uchaguzi wa Chama cha Makocha Tanzania (Tafca) kwa sababu wengi wao ni wanachama hivyo jambo ambalo limesababisha kushindwa kutekeleza baadhi ya mipango yao kwa wakati.

“Zipo sababu nyingi lakini kubwa ni kwamba baadhi ya wageni muhimu ambao walialikwa asilimia (80%) wameonyesha kutokuwepo kwa tarehe hiyo kwa sababu watakuwa nje ya jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya siku kuu za mwisho wa mwaka.

“Kwa kuzingatia uzito wa jambo lenyewe kamati imeona ni busara kusogeza mbele kwa siku 30 kwa lengo la kuwapa nafasi wahusika kwa pande zote mbili kuendelea na matayarisho hayo,” alisema Kakore.

Katika hatua nyingine, majina ya wanasoka walioingia fainali ya tuzo za mwakasoka bora wa mwaka yanatarajiwa kuwekwa wazi Januari mosi mwaka huu baada ya kukamilishwa kwa mchakato wa kupitia majina 93 yaliyokuwa yamependekezwa na wadau wa soka.

Mchakato wa kumpata mwanasoka bora wa mwaka ulianza tangu Agosti mosi mwaka huu ambapo wadau mbalimbali wa ndani ya nje ya Tanzania walipendekeza majina ya wachezaji ambao walistahili kutwaa tuzo hiyo.


Tuzo za Wzalendo zinalenga katika kuinua na kutambua mchango wa maendeleo ya soka la Tanzania kwa kipindi cha mwaka wa 2012 ambapo zitakuwa zikifanyika kila mwaka lengo likiwa ni kuendeleza na kuthamini kazi ambazo zimefanywa na wanasoka na wadau wa soka kwa muda wa mwaka mmoja.