Friday, May 21, 2010

Tuzo za nyota wa Tanzania zaja

Tuzo maalum kwa watu mbalimbali waliofanya mchango katika jamii ya watanzania zinatarajiwa kutolewa mwishoni mwa mwaka huu.

Mjumbe wa kamati ya tuzo hizo zenye heshima kubwa katika jamii ya Watanzania, David Mchome amesema kuwa libeneke hilo linatarajiwa kuchukua nafasi katika jiji la Dar es Salaam Desemba mwaka huu.

"Kila kitu kinakwenda sawa tunarajia kila kitu kitakwenda sawa, hii ni kutokana na ukweli kuwa watu wenye mchango katika jamii yetu wamesahaulika kitu ambacho ni hatari kwa taifa.

Kwa sasa kampuni ya Wazakendo bright media compani, inatarajiwa kufanya shughuli hiyo kwa niaba ya Watanzania wote ili kuifanya jamii iwakumbuke watu wenye majina makubwa katika taifa," alisema Mchome.

MRISHO MPOTO


ANNA KILANGO MALICELA


MRISHO NGASSA


PROF.ANNA TIBAIJUKA


watu wanaotarajiwa kupewa tunzo ni kama ifuatavyo:-

1.Mwanasiasa bora wa mwaka.
2.Mwanamuziki bora wa kiume wa mwaka.
3.Mwanamuziki bora wa kike wa mwaka.
4.Mwanamuziki bora chipukizi wa mwaka.
5.Mcheza filamu bora wa mwaka.
6.Mcheza filamu bora wa kike wa mwaka.
7.Mwanamichezo bora wa kiume wa mwaka.
8.Mwanamichezo bora wa kike wa mwaka.
9.Mwandishi bora wa michezo wa mwaka.
10.Mtangazaji bora wa mwaka.
11.Muimbaji bora wa kike wa muziki wa injili wa mwaka.
13.Muimbaji bora wa kiume wa muziki wa injili wa mwaka.
14.Filamu bora ya mwaka.
15.wimbo bora wa mwaka.

0 comments: