Saturday, February 19, 2011

kampeni ya madawa ya kulevya yaja






Taasisi ya kutoa elimu kwa wanafunzi na vijana juu ya adhari za madawa ya kulevya ya iitwayo (Youth Liberty Professional) imeandaa kampeni maalum kwa ajili ya kutoa elimu kwa vijana mashuleni.

Msemaji wa taasisi hiyo, Lovenes Sallu alisema kuwa wamejipanga kuhakikisha kuwa elimu hiyo inawafikia vijana wengi ambao wapo mashuleni na vyuoni.

Kampeni hiyo inajukana kama ‘fikiria Tanzania ya kesho’ inawahusu watu maarufu kama wanasiasa, wanasoka, wanamuziki na watu wengine waliopata mafanikio katika jamii ya Watanzania.

0 comments: