Monday, February 6, 2012

Rais Wa Zanzibar Dk Ali Shein Ashiriki Katika Sherehe Za Maulid Ya Kuzaliwa Bwana Mtume S.A.W


stadhi Salum Rashid wa Madrsa Qadiria ya Amani akisoma Maulid Barzanji Mlango wa nne,ambao Waislamu husimama na kumswalia Bwana Mtume,S.A.W,wakati wa sherehe za Maulid zilizofanyika jana katika Viwanja vya Maisara Suleiman Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,( katikati wakiitikia Dua katika sherehe za Maulid ya kuzaliwa Bwana Mtume S.A.W zilizofanyika jana katika viwanja vya Maisra Suleiman Mjini Zanzibar,ikiombwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabbi,(wa pili kushoto)(wa kwanza kulia) Jaji Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Othman Makungu,na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji,Wazri wa Katiba na Sheria Sheikh Abuu Bakar Khamis,(kushoto). (05/02/2012)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kushoto) akiwa katika sherehe za Maulid ya kuzaliwa Bwana Mtume S.A.W zilizofanyika jana katika viwanja vya Maisra Suleiman Mjini Zanzibar,(kushoto) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabbi,(wa kwanza kulia) Jaji Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Othman Makungu,na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji.Picha na Ramadhan Othman,IKULU-Zanzibar

0 comments: