Monday, February 6, 2012

Taswira Mbalimbali Za Rais Jakaya Kikwete Katika Sherehe Za Miaka 35 ya CCM Mwanza

Rais Jakaya Kikwete akihutubia maelfu ya wana CCM na wakaazi wa Mwanza leo katika kuadhimisha miaka 35 ya CCM uwanja wa Kirumba
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete wakiongoza matembezi hayo kutoka kwenye Ofisi ya CCM mkoa wa Mwanza hadi viwanja vya Furahisha jijini Mwanza akiwa na viongozi wa ngazi ya juu wa CCM. Kutoka Ofisi hiyo hadi kwenye viwanja ni umbali wa kilometa tatu.
Rais Kikwete akimsalimia Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Philip Mangula kabla yamatembezi kuanza Ofisi ya CCM mkoa wa Mwanza. Kulia ni Katibu Mkuu Mstaafu Yussuf Makamba.
Rais Kikwete akimsalimia Nape Nnauye Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kabla ya matembezi hayo.
Mama Salma Kikwete na Spika Anne Makinda na wakinamama wakisherehekea miaka 35 ya CCM baada ya kukunwa na wimbo wa Vicky kamata.Rais Jakaya Kikwete akiongoza matembezi ya mshikamano mapema asubuhi
Rais Jakaya Kikwete akisalimia vikundi mbalimbali vya burudani na wana CCM na wakaazi wa Mwanza leo katika kuadhimisha miaka 35 ya CCM uwanja wa Kirumba
wakaazi wa Mwanza leo katika kuadhimisha miaka 35 ya CCM uwanja wa Kirumba
wakaazi wa Mwanza wakiwa kwenye maandamano ya pikipiki katika kuadhimisha miaka 35 ya CCM uwanja wa Kirumba
Wageni mbalimbali walioudhuria sherehe za miaka 35 ya CCM uwanja wa Kirumba Mkoani Mwanza leo.Picha na IKULU

0 comments: