Tuesday, November 27, 2012

Chipukizi watesa Wazalendo awards 2012




KINYANG’ANYIRO cha kumpata mwanasoka bora wa mwaka 2012 katika tuzo za kila mwaka za Wazalendo, kimefikia pazuri baada ya majina ya wachezaji wachanga kuonekana kujitokeza zaidi ikilinganishwa na wale wenye umri mkubwa.

Mratibu wa tuzo hizo, Ahadi Kakore alisema kuwa tuzo za mwaka huu zimeonakana kuwa na msisimko mkubwa ambapo majina ya wachezaji wenye umri mdogo ndoyo yaliyopendekezwa zaidi ikilinganishwa na wakongwe.

“Tunafahamu kwamba kamati inaendelea na kazi yake ya kupembua majina lakini jambo kubwa lilionekana ni uwepo wa wachezaji wengi wachanga ikilinganishwa na wakongwe kitu ambacho kimeonekana kuwa ni cha tofauti.

“Ukiangalia uwiano yawachezaji wachanga na wakongwe ni dhahiri utaona kwamba kazi iliyopo  mbele ni kubwa katika kuhakikisha kuwa mambo yanakwenda sawa.

“Tunaimani kwamba angalau hadi kufikia tarehe za mwanzo za mwezi Desemba, tunaweza kujua mwelekeo kuwa nani ameingia na nani ameshindwa kuingia katika fainali.

“Kadhalika niwapongeze wote ambao wameendelea kutuunga mkono kwenye jambo hili kubwa katika maendeleo ya soka la Tanzania,” alisema Kakore.

Tunzo za Wazalendo zinatarajiwa kufanyika Desemba 30 mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo mshindi atapata tuzo, medali, cheti pamoja na fedha taslim.

0 comments: