Monday, October 15, 2012

ABDALLAH YUSUPH WA CLUB YA LUGALO ATWAA UBINGWA WA NMB MWALIMU NYERERE MASTERS GOLF




Mshindi wa mashindano ya gofu ya kumuenzi Mwl Nyerere Abdallah Yusuph toka klabu Lugalo akiwa na mgeni rasmi Jaji Mark Bomani na  Mkurugenzi wa wateja wakubwa wa benki ya NMB Kees Verbeek baada ya kutangwa mshindi kwenye hafla iliyofanyika juzi viwanja vya Gymkhana


Mashindando ya gofu ya kumuenzi Mwl JK Nyerere (Mwl Nyerere masters Golf) yaliyokuwa yanafadhiliwa na benki ya NMB  yaliyokuwa yanafanyika kwenye viwanja vya Gymkhana vya jijini Dar es salaam kuanzia jana yamefikia tamati leo kwa wachezaji mbalimbali kukabidhiwa zawadi zao huku mchezaji wa klabu ya Lugalo Abdallah Yusuph Idd akiibuka mchezaji wa jumla.

Mshiriki Abdallah Yusuph toka club ya Lugalo alitawazwa kuwa bingwa wa gofu ya kumuenzi mwalimu Nyerere mwaka 2012

Akifunga mashindano hayo ambayo yalikuwa yameshirikisha wachezaji zaidi ya 150 toka klabu mbalimbali za gofu Tanzania Mark Bomani ambaye ni Mkurugenzi wa bodi ya Kiwanda cha bia ya Serengeti alisema wachezaji wanatakiwa kumuenzi Mwl Nyerere kwa kuendeleza yale yote ambayo mwalimu aliyaacha.

Wachezaji wa umri mbalimbali kuanzia junior hadi elders walikabidhiwa zawadi zao,

Naye Mkurugenzi wa wateja wakubwa wa benki ya NMB Kees Verbeek alisema benki yake inafuraha kudhamini mashindano hayo kwa sababu inathamini yale ambayo mwalimu ambaye ni mwasisi wa taifa la Tanzania aliyoaacha kwani ndio maana na wao wanaweza kuwekeza maana mwalimu katuacha amani.

Nao wachezaji walioshiriki walisema mashindano yalikuwa mazuri na ushindani ni mkubwa kwani watu wameahamasika kujifunza kucheza gofu

0 comments: