Sunday, October 7, 2012

AZAM YAIPIGIA HONI SIMBA

 
Ligi kuu ya soka Tanzania Bara iliendelea jana  kwa michezo miwili kuchezwa katika viwanja viwili tofauti.
Katika uwanja wa Azam Complex Chamazi ,Azam fc imefanikiwa kupata points zote tatu muhimu baaada ya kuifunga Afrikan Lyon kwa bao 1-0 lililofungwa na John Boko baada ya kupata pasi ya Kipre Tcheche aliyeunasa mpira uliomtoka mlinda mlango wa Lyon.
Matokeo hayo yameifanya Azam kufikisha jumla ya points 13 sawa na Simba ambao ndio mabingwa watetezi wa taji la ligi hiyo na ambao kesho watakuwa wakishuka dimbani kucheza dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha mchezo ambao utachezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mchezo mwingine uliochezwa leo ni baina ya Ruvu Shooting ya Pwani waliokuwa wenyeji wa Coastal Union ya Tanga mchezo ambao umefanyika katika uwanja wa Mabatini Mlandizi.
Katika mchezo huo wenyeji JKT Ruvu wamefanikiwa kuchomoza na ushindi wa mabao 2-0, matokeo ambayo yamewafanya Ruvu kufikisha jumla ya points 9 na hivyo kukalia nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo.

0 comments: