This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Friday, October 26, 2012

Press Release




Press Release
CHAMA CHA MSALABA MWEKUNDU MKOA WA  DAR ES SALAAM: VOLUNTEERS NA WANACHAMA,
SLP 1133,
DAR ES SALAAM.






WANACHAMA YAH: PINGAMIZI DHIDI YA MAJINA YA BAADHI YA WAGOMBEA WA NAFASI ZA UONGOZI WA CHAMA  CHA MSALABA MWEKUNDU MKOA WA   DAR ES SALAAM WASIO NA VIGEZO.


Chama cha Msalaba Mwekundu mkoa wa  Dar es Salaam: Volunteers na Wanachama, kwa masikitiko makubwa, tunapenda kuelezea malalamiko yetu  juu ya kukiukwa kwa taratibu za uchaguzi mkuu wa chama Mkoa wa Dar es Salaam.

Kama wanachama, tunasikitika kuona baadhi ya taratibu za msingi zinakiukwa kwa makusudi ili hali ni kinyume na taratibu zinazoongoza chama chetu hasa taratibu zinazosimamia uchaguzi mkuu.

Jambo ambalo linatusikitisha zaidi ni namnba ambavyo baadhi ya viongozi wetu wameshindwa kusaidia katika suala hili ambalo kiukweli linaweza kurudisha nyuma hatarakati na maana halisi chama katika kusaidia jamii inayotuzunguka.

Tatizo ambalo sisi wanachama tunalilalamikia ni namna taratibu zilizoendesha mchakato wa zoezi zima la kuyakusanya na kuyachambua majina ya wanachama walioomba nafasi mbali mbali za uongozi ngazi ya Mkoa wa Dar Es Salaam na hatimaye siku chache zilizopita  kuyatangaza  majina ya wagombea waliofuzu vigezo hivyo.

Uchaguzi huu wa mwaka 2012 ambao kimsingi unakua wa kwanza kufanyika chini ya kanuni mpya za uchaguzi zilizopitishwa na Bodi mwaka 2011.

Tofauti na miaka mingine, kanuni hizi zimejikita zaidi katika kigezo cha elimu ya mgombea, mafunzo na ujuzi katika fani husika kwa mfano; ngazi ya Matawi na Wilaya  mgombea lazima awe na elimu ya kidato cha nne, Mkoani lazima awe na elimu isiyopungua kidato cha sita na Taifa awe na shahada ya kwanza.


Pamoja na kanuni hizo za wazi, lakini badi zimeshindikana kufanyika, tunadhani kanuni hizo hazikuzingatia kanuni kuu saba za msalaba mwekundu. 

Baadhi ya wagombea waliopitishwa kugombea nafasi hizo tunaamini wazi kuwa hawakustahili kwa kuzingatia kigezo cha elimu kwamba hawakufikia elimu iliyokuwa inahistajika kwa ngazi ya mkoa,  (yaani hawana elimu ya kidato cha sita) na kuwaacha wale wenye sifa hizo na nyinginezo.

Majina hayo ni  Amina Mwalimu  (Mafunzo na Uuguzi), Hidan Ricco  (Makamu Mwenyekiti), Subira Tamla (Mafunzo na Uuguzi), Edson Kanisa (Maafa na Habari)  Mayasa Bashele (Jinsia) Francis Msisi (Maafa na Habari).

Kutokana na makosa hayo ndiyo maana tunaona kuna sababu ya uchaguzi huo kusimamishwa  badala ya kufanyika Oktoba 27 mwaka 2012 ili kutoa nafasio kwa mchakato huo  kufanyika kwa upya kwa ajili yan kuitendea hali taasisi kutokana na heshima kubwa iliyonayo mbele ya jamii. 

pia tunaambatanisha na barua ambayo tulimwandikia Mwenyekiti wa Taifa  ya Oktoba 16 2012 na nakala kumpatia Katibu Mkuu Chama Cha Msalaba Mwekundu Taifa.

Sunday, October 21, 2012

YANGA HIYOO NAFASI YA 3 BAADA YA KUIFUNGA RUVU SHOOTING 3-2



TIMU ya Yanga jana ilishinda 3-2 dhidi ya Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huu unaifanya Yanga ifikishe pointi 14, baada ya kucheza michezo nane na kujiweka katika nafasi ya tatu huku ikizidwa pointi tatu na Azam inayoshika nafasi ya pili na pointi nne na wapinzani wao wa jadi Simba inayoongoza ligi hiyo.

Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa timu zote kutoshana nguvu kwa mabao 2-2, Ruvu Shooting wakitangulia kufunga na kusawazisha.

Mabao ya Ruvu yalifungwa na mshambuliaji Seif Abdallah dakika ya tatu na lingine dakika ya 10.

Mabao ya Yanga yalifungwa na Mbuyi Twite dk 20 baada ya Rashid Gumbo kufanyiwa faulo nje ya eneo penalti na bila ajizi beki huyo wa Yanga aliyetokea APRkupiga shuti kali lililomshinda golikipa Benjamin Haule.

Jeryson Tegete alifunga bao la pili baada ya kuunganisha krosi nzuri aliyopiga Juma Abdul dakika ya 36.

Bao la tatu lilifungwa dk 65 na Didier Kavumbagu kipindi cha pili.

Baadae Ruvu shooting walizinduka na kufanya mashambulizi ambayo yalisababisha kosa kosa langoni mwa Yanga lakini bahati haikuwa yao kwan mpaka mwamuzi anapuliza filimbi ya kumaliza mchezo mabao yalikuwa 3-2

Kikosi cha Yanga ni; Yaw Berko, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Mbuyu Twite, Rashid Gumbo, Nurdin Bazkari, Haruna Niyonzima, Jerry Tegete, Didier Kavumbangu na David Luhende.

Ruvu Shooting; Benjamin Haule, Michael Aidan, Baraka Jaffari, George Assey, Ibrahim Shaaban, Ernest Ernest, Raphael Kyala, Hassan Dilunga, Seif Abdallah, Abrahman Mussa na Said Dilunga.

Kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Coastal Union imeifunga Mtibwa Sugar mabao 3-1, wafungaji wa Coastal Union ni Juma Jabu, Daniel Lyanga na Lameck Dayton huku la Mtibwa likifungwa na Shaaban Nditi.

YANGA YAKABIDHIWA JEZI YENYE NEMBO YA MDHAMINI WALIYOITAKA

Meneja Mahusiano ya Nje wa kampuni ya Sima za mkononi VODACOM, Salum Mwalimu akionesha jezi walizokabidhi kwa klabu ya Yanga zikiwa na doa jeusi.


 Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Laurence Mwalusako (kati) akipokea jezi walizokabidhiwa na Vodacom zikiwa na doa jeusi kutoka kwa Meneja Mahusiano ya Nje wa kampuni ya Sima za mkononi VODACOM, Salum Mwalimu (kushoto). Kulia ni Ofisa Udhamini wa kampuni hiyo, Ibrahim Kaude

Friday, October 19, 2012

KAMATI YA UCHAGUZI YA TFF

 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 
MAAMUZI KUHUSU  RUFAA DHIDI YA MAAMUZI YA KAMATI ZA UCHAGUZI VYAMA VYA MPIRA WA MIGUU MKOA WA MBEYA (MREFA), MKOA WA SHINYANGA (SHIREFA) NA MKOA WA DAR ES SALAAA (DRFA).
 
19 OKTOBA 2012
 
 
1.                   Kwa mujibu wa Katiba ya TFF Ibara ya 49(1), Kanuni za Uchaguzi  za wanachama wa TFF, Ibara  ya  10(6), 12(1) na 26(2) na (3), Kamati ya Uchaguzi ya TFF katika vikao vyake vilivyofanyika tarehe 12 na 18 Oktoba 2012 ilijadili michakato ya chaguzi za vyama vya mpira wa miguu vya Mikoa ya Mbeya (MREFA), Shinyanga (SHIREFA) na  Dar es Salaam (DRFA) na  kutoa maamuzi kama ifuatavyo:
 
(a)                 Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA)
 
(i)                  Rufaa ya Ndg. Charles Makwaza: Kamati ilijadili rufaa iliyowasilishwa na Ndg. Charles Makwaza dhidi ya Kamati ya Uchaguzi ya MREFA, iliyoomba Kamati ya Uchaguzi ya TFF kubatilisha uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya MREFA kumpitisha Ndg. John Mwamwaja kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa MREFA, kwamba hakutekeleza wajibu wa kikatiba wa kuitisha Mkutano Mkuu wa MREFA kwa muda wa miaka 3.
 
Baada ya kupitia maelezo ya warufani na warufaniwa, Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilijiridhisha kuwa vielelezo na maelezo ya Ndg. Charles Makwaza yaliyowasilishwa mbele ya Kamati kwa kiwango kikubwa hayakuwa ya kweli. Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeitupa rufaa hiyo.
 
(ii)                Rufaa ya Ndg. Lusekelo E. Mwanjala: Kamati ilijadili rufaa iliyowasilishwa na Ndg. Lusekelo E. Mwanjala ikipinga  maamuzi ya  Kamati ya Uchaguzi ya MREFA kuliondoa jina lake kugombea  nafasi ya Mwenyekiti wa MREFA, kwa kigezo cha kutokuwa na uzoefu wa uongozi wa mpira wa Miguu.
 
Kamati ilipitia vielelezo kuhusu rufaa na kujadili maelezo ya Mrufani na Mrufaniwa na ilijiridhisha kuwa Ndg. Mwanjala anakidhi kigezo cha uzoefu. Kamati inakubaliana na rufaa ya mrufaa dhidi ya maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya MREFA na hivyo imemrejesha Ndg. Mwanjala kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa MREFA. 
 
 
(iii)              Rufaa ya Ndg. Thadeo T. Kalua: Kamati ilijadili rufaa iliyowasilishwa  mbele yake na Ndg. Kalua ikipinga  maamuzi ya  Kamati ya Uchaguzi ya MREFA kuliondoa jina lake kugombea  nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF, kwa kigezo cha kutokuwa Mkazi wa Mkoa wa Mbeya. Kamati ilipitia vielelezo kuhusu rufaa hii na kubaini kuwa Katiba ya MREFA iliyosajiliwa haina sharti hilo kwa waombaji uongozi.  Kamati inakubaliana na maombi ya
 
 
(iv)               mrufaa na inamrejesha Ndg. Thadeo Kalua kugombea nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF. 
 
(v)                 Uchaguzi wa MREFA utafanyika Jumamosi, tarehe 27 Oktoba 2012 kama ulivyopangwa.
 
 
(b)                Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Shinyanga (SHIREFA).
 
(i)                   Rufaa ya Ndg. Ibrahim Magoma: Kamati ilijadili rufaa iliyowasilishwa na Ndg. Magoma ikipinga maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya SHIREFA kuliondoa jina lake kugombea nafasi ya Katibu wa SHIREFA, kwa kigezo cha kuingilia Mchakato wa Uchaguzi kunyume na Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF na pia kutozingatia matakwa ya Kanuni hizo katika kujaza fomu za maombi ya uongozi wa SHIREFA.
 
Kamati ilipitia vielelezo kuhusu rufaa ya Ndg. Magoma na kujadili maelezo ya Mrufani na Mrufaniwa na ilijiridhisha kuwa Ndg. Magoma  aliingilia mchakato wa uchaguzi wa SHIREFA kunyume na Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF akiwa Katibu Mkuu wa SHIREFA kwa kushiriki kuivunja Kamati ya Uchaguzi ya SHIREFA iliyokuwa ikendelea na mchakato wa uchaguzi wa SHIREFA.  Kamati inakubaliana na uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya SHIREFA wa kumwondoa Ndg. Magoma kugombea nafasi ya Katibu wa SHIREFA.  Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeitupa rufaa hiyo.
 
(ii)                 Uchaguzi wa SHIREFA umesogezwa Mbele kwa siku nne. Uchaguzi huo utafanyika Alhamisi, tarehe 25 Oktoba 2012, mjini Shinyanga.
 
 
(c)                 Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es salaam (DRFA).
 
Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilijadili Mchakato wa Uchaguzi wa DRFA na rufaa dhidi ya maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya DRFA  na kuamua kama ifuatavyo:
 
(i)                   Marekebisho na usajili wa Katiba ya DRFA: Hoja ya rufaa iliwasilishwa na Ndg. Michael R. Wambura ilikihoji uhalali wa marekebisho na usajili wa Katiba ya DRFA, kwamba usajili wa Katiba ya DRFA si halali. Kamati ilibaini kuwa marekebisho ya Katiba hiyo yalifanyika kwa kufuata maagizo ya TFF na kwamba DRFA ilizingatia maagizo hayo. Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliridhika kuwa Katiba ya DRFA imesajiliwa na Msajili wa vyama na vilabu vya michezo baada ya kuridhiwa na TFF, na hivyo, Kamati iliitupa hoja hiyo ya Mrufani kuhusu uhalali na usajili wa Katiba ya DRFA.
 
(ii)                 Kuundwa kwa Kamati ya Uchaguzi ya TFF : Hoja ya rufaa ya Ndg. Michael R. Wambura iliomba Kamati ya Uchaguzi ya TFF kutoa tamko kuwa Kamati ya Uchaguzi ya DRFA imeundwa bila kufuata Kanuni za Uchaguzi Ibara ya 3(2). Kamati iliridhika kuwa Kamati ya Uchaguzi ya DRFA iliteuliwa kabla ya marekebisho ya Kanuni za Uchaguzi  za wanachama wa TFF hususan, Ibara ya 3(2), hivyo uteuzi wa wajumbe wa Kamati hiyo haukukiuka Kanuni za Uchaguzi. Kamati iliitupa rufaa hiyo.
 
(iii)                Wapiga kura wa Mkutano Mkuu wa DRFA: Hoja za rufaa za Ndg. Michael R. Wambura na Ndg. Juma Jabir ziliomba kuyaondoa majina ya Ndg. Abeid Mziba, Ndg. Salehe Ndonga, Peter Muhinzi na Ndg. Daudi Kanuti katika orodha ya wapiga kura wa Mkutano Mkuu wa DRFA na uongozi wa wanachama wa DRFA, kwamba hawana sifa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi na Katiba za wanachama wa DRFA. Kamati ya Uchaguzi ya TFF haikupata vielelezo kuhusu hoja iliyowasisilishwa mbele ya Kamati na hivyo kuitupa hoja hiyo ya mrufani.
 
(iv)               Rufaa dhidi ya Ndg. Mohamed Salim (Bakhressa) kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa DRFA.  Rufaa dhidi ya uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya DRFA wa kumpitisha Ndg. Amin Mohamed Salim (Bakhressa) kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa DRFA iliyowasilishwa na Ndg. Michael R. Wambura na Ndg. Juma Jabir iliomba jina la Ndg. Amin Mohamed Salim (Bakhressa) liondolewe katika orodha ya wagombea uongozi wa DRFA kwa nafasi ya Mwenyekiti, kwa kuwa hana elimu ya kiwango cha kidato cha nne na hivyo kutokidhi matakwa ya Katiba ya DRFA Ibara ya 29(2) inayotamka kwamba ‘Mtu yeyote anayegombea nafasi yoyote ya DRFA hana budi awe na kiwango cha elimu kisichopungua kidato cha nne (Academic Certificate of Ordinary Secondary Education).
 
Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilipitia vielelezo kuhusu rufaa dhidi ya maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya DRFA na kujadili maelezo ya Warufani, Kamati ya Uchaguzi ya DRFA na Ndg. Amin Mohamed Salim na ilijiridhisha kuwa Ndg. Amin Mohamed Salim (Bakhressa) hana elimu ya kiwango cha kidato cha nne na hivyo hakidhi matakwa ya Katiba ya DRFA Ibara 29(2). Kwa kutokidhi matakwa hayo ya katiba ya DRFA, Ndg. Amin Mohamed Salim (Bakhressa) hastahili kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa DRFA. Kamati ya Uchaguzi ya TFF inakubaliana na maombi ya Warufaa.
 
(v)                 Rufaa kupinga kuenguliwa kugombea Uongozi DRFA:  Ndg. Evans Elieza na Ndg. Juma Jabir waliwasilisha rufaa  wakiomba Kamati ya Uchaguzi ya TFF kutengua uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya DRFA wa kuwaengua kugombea uongozi kwa madai ya kugushi sahihi ya Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kinondoni (KIFA). Katika vielelezo mbalimbali vilivyoletwa mbele ya Kamati na baada ya kuwahoji warufani, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya DRFA, Katibu wa KIFA, Ndg. Seif Ally Mailo aliyeshuhudia maelezo ya fomu za waombaji uongozi DRFA na baadhi ya waombaji uongozi ambao kupitishwa kwao na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA kulilalamikiwa, Kamati ilibaini kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa Kanuni na taratibu za uchaguzi zilizofanywa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA na pia ama KIFA au wagombea wenyewe. Kutokana na mkanganyiko, maelezo yenye utata kutoka kwa warufani na warufaniwa na maamuzi ya utata ya Kamati ya Uchaguzi ya DRFA yameufanya mchakato wa uchaguzi wa DRFA kupoteza hadhi ya uchaguzi unaozingatia Kanuni za Uchaguzi na misingi ya demokrasia na uwazi kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni za Uchaguzi za TFF. Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilijiridhisha kwamba:
 
·         Kamati ya Uchaguzi ya DRFA iliwapitisha wagombea Ndg. Gungurugwa Tambaza, Ndg. Mohammed Bhinda, Ndg. Benny Kisaka na Ndg. Hamisi Ayoub Mpapai bila kuwa na vielelezo vinavyothibitisha kuwa wana kiwango cha elimu kisichopungua kidato cha nne (Academic Certificate of Ordinary Secondary Education).
 
·         Hoja ya kughushi saini ya Katibu wa KIFA katika kushuhudia maelezo ya  baadhi ya wombaji uongozi, ambayo  ilitumiwa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA kuwaondoa kugombea uongozi waombaji uongozi watano (5)  Ndg. Hamis Ambar, Ndg. Hamisi Kisiwa, Ndg. Andrew Tupa, Ndg. Evans Elieza na Ndg. Juma Jabir  haikutumika kuwaondoa baadhi wagombea ingawa fomu za waombaji uongozi saba zilisainiwa na Ndg.  Ndg. Seif Ally Mailo.
 
·         Ndg. Seif Ally Mailo ambaye si mwajiriwa na si kiongozi wa KIFA hakuwa na mamlaka ya kushuhudia maelezo ya wagombea kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi.
 
·         Kulikuwa na hali ya kumficha Ndg. Seif Ally Mailo aliyesaini fomu za wagombea walioenguliwa kwa kigezo cha kughushi saini asifike kwenye kamati ya Uchaguzi ya TFF kutoa maelezo kuhusu ushiriki wake katika mchakato wa uchaguzi wa DRFA.
 
·         Fomu za wagombea Ndg. Said H.Tully na Ndg. Shaffih Dauda zilizojadiliwa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA na hivyo kupitishwa na Kamati hiyo zilichezewa (tempered-with) kwa kunyofolewa baadhi ya kurasa na kuwekwa kurasa zenye maelezo na saini ambazo si za Ndg. Said H.Tully na Ndg. Shaffih Dauda. Wagombea hao ambao walikuwa wamepetishwa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA kwa maelezo kwamba fomu zao zilikuwa zimeshudiwa kwa sahihi halali ya Ndg. Ndg. Seif Ally Mailo
 
 
 
walikana kwa maandishi na kutoa vielelezo vilivyothibitisha kwamba fomu zao zilichezewa na maelezo yaliyo kwenye kurasa zilizobadilishwa siyo wao walioyandika na kusaini.
 
·         Kamati ya Uchaguzi ya DRFA iliwaondoa baadhi ya waombaji uongozi kwa maelezo kwamba maelezo kwenye fomu za wagombea hao hayakushuhudiwa na viongozi vyama wanachama wa DRFA wenye mamlaka ya kushuhudia maelezo ya waombaji uongozi lakini bila kuzingatia matakwa hayo ya kikanuni ikawapitisha kugombea Ndg. Muhsin S. Balhabou na Ndg. Benny Kisaka ambao maelezo ya kwenye fomu zao hayakushuhudiwa na kiongozi wa chama mwanachama yeyote wa DRFA.
 
·         Kamati ya Uchaguzi ya DRFA inahusika kwa kiwango kikubwa katika ukiukwaji wa Kanuni na taratibu za uchaguzi na kutozingatia matakwa ya Katiba ya DRFA katika mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa DRFA.
 
Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuzingatia Katiba ya TFF Ibara ya 49(1), Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF Ibara  ya  10(6), 12(1) na 26(2) na (3):
 
(i)                   Imeifuta Kamati ya Uchaguzi ya DRFA. DRFA inaagizwa kuteuwa Kamati mpya ya Uchaguzi itakayoandaa na kutekeleza majukumu yake ikizingatia Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF na Katiba ya DRFA. Uteuzi wa Kamati mpya ya Uchaguzi ya DRFA ufanyike kabla ya tarehe 25 Oktoba 2012
 
(ii)                 Imefuta mchakato wa Uchaguzi wa DRFA. Mchakato wa uchaguzi utaanza upya tarehe 29 Oktoba 2012 na uchaguzi utafanyika tarehe 08 Desemba 2012. Wagombea wote waliokuwa wamelipia Fomu za maombi ya uongozi (Fomu Na. 1) wanaokidhi sifa za kugombea uongozi kwa mujibu wa Katiba ya DRFA na Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF wajaze upya Fomu Na.1 bila kutozwa ada kwa nafasi zinazoendana na zile walizokuwa wameomba kugombea.
 
 
 
 
Deogratias Lyatto
MWENYEKITI
KAMATI YA UCHAGUZI TFF
 
 
 
 
 

YANGA, SHOOTING SASA KUCHEZA TAIFA


Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kati ya Yanga na Ruvu Shooting uliopangwa kuchezwa kesho (Oktoba 20 mwaka huu) Uwanja wa Chamazi sasa umehamishiwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.15 jioni.
 
Mabadiliko hayo yamefanyika kutokana na maombi ya timu hizo mbili kutaka mechi ichezwe Uwanja wa Taifa kutokana na sababu mbalimbali ambazo zimeridhiwa na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikiwemo siku hiyo uwanja huo kutokuwa na mechi.
 
Viingilio katika mechi hiyo itakayokuwa chini ya mwamuzi Amon Paul kutoka Mara ni sh. 5,000 viti vya kijani na bluu, sh. 8,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP B na C na sh. 20,000 kwa VIP A.
 
Pia Kamati ya Ligi imekataa ombi la timu ya Azam kutaka mechi zake za nyumbani za ligi hiyo zichezwe dhidi ya Simba na Yanga zichezwe Uwanja wa Chamazi kutokana na sababu za kiusalama.
 
Nayo Coastal Union itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar katika mechi nyingine ya ligi hiyo itakayochezwa kesho (Oktoba 20 mwaka huu) katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
 
Mchezo huo namba 56 wa kukamilisha raundi ya nane utachezeshwa na mwamuzi Israel Nkongo atakayesaidiwa na Hamis Chang’walu na Omari Kambangwa, wote kutoka Dar es Salaam.
 
Ligi hiyo itaendelea tena Jumapili (Oktoba 21 mwaka huu) kwa mechi tatu. JKT Ruvu itaoneshana kazi na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Chamazi, Mgambo Shooting itaikaribisha Simba kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati Tanzania Prisons na Toto Africans zitapimana ubavu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
 
TWFA YATAKA ORODHA YA WAPIGA KURA
Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) chini ya Mwenyekiti wake Ombeni Zavala imewataka wanachama wa TWFA ambao ni mikoa ya Tanzania Bara kuwasilisha orodha ya wajumbe wao wa mkutano wa uchaguzi.
 
Wajumbe wenye sifa ya kuhudhuria Mkutano wa TWFA ni kutoka vyama vya mikoa ambavyo tayari vimefanya uchaguzi. Wajumbe hao ni Mwenyekiti, Katibu na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TWFA.
 
Mikoa ambayo imeshafanya uchaguzi mpaka sasa ni Iringa, Kigoma, Mwanza, Pwani na Tanga. Mikoa ambayo bado inahimizwa kufanya uchaguzi, na mwisho wa kutuma majina ya wajumbe kwa Mwenyekiti Zavala ni Oktoba 25 mwaka huu.
 
Mkoa ambao utakuwa haujafanya uchaguzi utakuwa umenyimwa haki ya kushiriki uchaguzi wa TWFA utakaofanyika Novemba 4 mwaka huu.
 
MTANZANIA AOMBEWA ITC ACHEZE MAREKANI
Mchezaji Millan Mbise kutoka Tanzania ameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) itakayomwezesha kucheza mpira wa miguu nchini Marekani.
 
Shirikisho la Mpira wa Miguu la Marekani (USSF) limemuombea hati hiyo Mbise kama mchezaji wa ridhaa ili ajiunge na timu ya Virginia Youth Soccer.
 
Klabu ya zamani ya Mbise aliyezaliwa Agosti 18, 1994 imetajwa kuwa Super Sport FC, na mechi ya mwisho kwenye timu hiyo alicheza Novemba 15 mwaka juzi.
 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanya mawasiliano na pande husika kabla ya kutoa hati hiyo kwa mchezaji huyo kama ilivyoombwa na shirikisho hilo la Marekani.
 
TASMA WAANZA MCHAKATO WA UCHAGUZI
Chama cha Madaktari wa Tiba ya Michezo Tanzania (TASMA) leo (Oktoba 19 mwaka huu) kimetangaza kuanza mchakato wa uchaguzi wa chama hicho uliopangwa kufanyika Novemba 28 mwaka huu.
 
Kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TASMA, Dk. Francis Mchomvu, fomu kwa wanamichezo wanaotaka kugombea uongozi wa chama hicho zitaanza kutolewa Oktoba 21 mwaka huu.
 
Mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu hizo zinazopatikana ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ni saa 10.00 alasiri ya Oktoba 26 mwaka huu. Ada ya fomu kwa nafasi nne za juu ni sh. 200,000 wakati kwa nafasi nyingine zilizobaki ni sh. 100,000. Kati ya Oktoba 27-31 mwaka huu Kamati ya Uchaguzi ya TASMA itapitia fomu na kutangaza majina ya waliojitokeza kuomba uongozi.
 
Nafasi zitakazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mhazini, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF na wajumbe wawili wa Kamati ya Utendaji.
 
Kipindi cha pingamizi kwa waombaji ni kuanzia Novemba 1-6 mwaka huu, na pingamizi zinatakiwa kuwasilishwa kwa Katibu wa Kamati ya Uchaguzi ya TASMA kabla ya saa 10.00 alasiri ya Novemba 6 mwaka huu. Hakuna ada kwenye pingamizi.
 
Pingamizi zitajadiliwa na kufanyiwa uamuzi kati ya Novemba 7-9 mwaka huu. Usaili utafanyika kati ya Novemba 10-11 mwaka huu ambapo matokeo ya usaili huo vilevile yatatangazwa ili kutoa fursa kwa rufani ambazo zinatakiwa kukatwa kati ya Novemba 11-13 mwaka huu.
 
Rufani ambazo zinaambatana na ada y ash. 500,000 zinatakiwa kufikishwa kwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kabla ya saa 10.00 alasiri ya Novemba 13 mwaka huu.
 
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Thursday, October 18, 2012

SIMBA NA KAGERA HAKUNA MBABE





TIMU ya Simba jana ilitoka sare ya 2-2 na Kagera Sugar katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa matokeo hayo, Simba imefikisha pointi 18 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu, kutokana na Azam FC kulazimishwa sare ya bila kufungana na Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Hadi mapumziko, Simba SC walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na mshambuliaji wa kimataifa raia wa Zambia, Felix Mumba Sunzu Jr. dakika ya nane, akiunganisha kwa kichwa krosi ya Nassor Masoud ‘Chollo’ kutoka wingi ya kulia.

Kipindi cha pili Simba ilirudi na moto tena na katika dakika ya 51, Mrisho Khalfan Ngassa aliifungia timu hiyo bao la pili kwa shuti kali lililowababatiza mabeki wa Kagera Sugar kutinga nyavuni.

Baada ya hapo, Kagera walizinduka na kuanza kulishambulia lango la Simba kupitia pembeni na dakika ya 64 Themi Felix aliunganisha kwa kichwa krosi ya George Kavilla na kuifungia Kagera bao la kwanza.

Bao liliwazindua Kagera, ambao waliongeza kasi ya kushambulia lango la Simba na dakika ya 66, Juma Nyosso alimkwatua kwenye eneo la penalti Paul Ngwai na Salum Kanoni akaenda kupiga penalti, akiisawazishia Kagera.

Baada ya hapo timu zilianza kushambuliana kwa zamu na mpira ulikuwa mzuri zaidi kutokana na mashambulizi ya pande zote mbili.

Katika mechi nyingine, Mgambo imeifunga Toto African 2-0 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

JKT Ruvu imezinduka baada ya kuifunga Polisi Morogoro 2-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro

JKT Oljoro imetoka 0-0 na African Lyon.

Simba SC; Juma Kaseja (Nahodha), Nassor Masoud ‘Chollo’, Amir Maftah, Paschal Ochieng, Juma Nyosso, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Haruna Moshi, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi na Mrisho Ngassa.

Kagera Sugar; Andrew Ntala, Salum Kanoni, Martin Muganyizi, Amandus Nesta (Nahodha), Benjamin Effe, Malegesi Mwangwa, Daudi Jumanne, George Kavilla, Shijja Mkina, Enyinna Darlington na Wilfred Ammeh.

Tuesday, October 16, 2012

SIMBA YAANZIA RAUNDI YA NANE NA KAGERA SUGAR

Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi nane kesho (Oktoba 17 mwaka huu) kwa mechi tano huku vinara wa ligi hiyo Simba wakiialika Kagera Sugar kutoka mkoani Kagera kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
Mechi hiyo namba 52 itachezeshwa na mwamuzi Ronald Swai kutoka Arusha wakati waamuzi wasaidizi ni Julius Kasitu na Methusela Musebula, wote kutoka Shinyanga. Mwamuzi wa akiba ni Ephrony Ndisa wa Dar es Salaam huku mtathimini wa waamuzi akiwa Charles Mchau kutoka Moshi.
 
Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Tanzania Prisons inayofundishwa na Jumanne Chale na Azam iliyo chini ya kocha Boris Bunjak kutoka Serbia. Nayo Polisi Morogoro iliyopanda msimu huu itakuwa mwenyeji wa JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Jamhuri.
 
Mgambo Shooting ambayo imepata ushindi mara mbili mfululizo itakuwa nyumbani Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga ikiikaribisha Toto Africans katika mechi itakayochezeshwa na Geofrey Tumaini wa Dar es Salaam. Oljoro JKT inayonolewa na Mbwana Makata itakuwa nyumbani Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha dhidi ya African Lyon.

TAFCA YAONGEZA MUDA WA KUCHUKUA FOMU

Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) imeongeza muda kwa wagombea kuchukua fomu kwa ajili ya uchaguzi wa chama hicho ambao sasa utafanyika Novemba 25 mwaka huu.
 
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TAFCA, Ramadhan Mambosasa, jana ndiyo ilikuwa mwisho wa kuchukua fomu lakini mwitikio wa wagombea bado umekuwa mdogo ambapo ni watano tu waliojitokeza.
 
Hivyo, amesema wameongeza muda wa kuchukua na kurudisha fomu ambapo mwisho itakuwa ni Oktoba 19 mwaka huu saa 10 kamili alasiri. Fomu zinapatikana ofisi za TAFCA ambazo ziko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
 
Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF, Mhazini na wajumbe watatu wa Kamati ya Utendaji.
 

DARAJA LA KWANZA KUANZA OCTOBA 24

Michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ya Tanzania Bara inaanza rasmi Oktoba 24 mwaka huu kwa timu 18 kati ya 24 kujitupa kwenye viwanja tisa tofauti katika ligi hiyo inayochezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
 
Mechi za raundi ya kwanza za kundi A zitakazochezwa Oktoba 24 mwaka huu ni Burkina Faso dhidi ya Mbeya City (Jamhuri, Morogoro), Mlale JKT na Small Kids (Majimaji, Songea) na Kurugenzi Mufindi dhidi ya Majimaji (Uwanja wa Wambi, Mufindi mkoani Iringa).
 
Mkamba Rangers na Polisi Iringa zitakamilisha raundi ya kwanza kwa kundi hilo Oktoba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
 
Mechi za raundi ya pili kwa kundi hilo zitachezwa Oktoba 27 mwaka huu kwa Polisi Iringa vs Mbeya City (Samora, Iringa), Majimaji vs Small Kids (Majimaji, Songea), Burkina Faso vs Mkamba Rangers (Jamhuri, Morogoro) na Kurugenzi Mufindi vs Mlale JKT (Wambi, Mufindi).
 
Raundi ya tatu ni Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Mbeya City vs Mlale JKT (Sokoine, Mbeya), Small Kids vs Mkamba Rangers (Nelson Mandela, Sumbawanga), Majimaji vs Burkina Faso (Majimaji, Songea) na Polisi Iringa vs Kurugenzi Mufindi (Samora, Iringa).
 
Kundi B Oktoba 24 mwaka huu ni Ndanda vs Transit Camp (Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara), Villa Squad vs Moro United (Mabatini, Pwani) wakati Oktoba 25 mwaka huu ni Green Warriors vs Tessema (Mabatini, Pwani) na Polisi Dar es Salaam vs Ashanti United (Chamazi, Dar es Salaam).
 
Raundi ya pili kwa kundi hilo ni Oktoba 27 mwaka huu Ndanda vs Green Warriors (Nangwanda Sijaona, Mtwara), Villa Squad vs Tessema (Mabatini, Pwani) wakati Oktoba 28 mwaka huu ni Ashanti United vs Transit Camp (Mabatini, Pwani) na Oktoba 29 mwaka huu ni Moro United vs Polisi Dar es Salaam (Chamazi, Dar es Salaam).
 
Novemba 1 mwaka huu ni Green Warriors vs Ashanti United (Mabatini, Pwani), Novemba 2 mwaka huu ni Polisi Dar es Salaam vs Villa Squad (Chamazi, Dar es Salaam), Novemba 4 mwaka huu ni Tessema vs Ndanda (Chamazi, Dar es Salaam) na Transit Camp vs Moro United (Mabatini, Pwani).
 
Kundi C ni Oktoba 24 mwaka huu Kanembwa FC vs Polisi Dodoma (Lake Tanganyika, Kigoma), Mwadui vs Morani (Kambarage, Shinyanga), Pamba vs Polisi Mara (Kirumba, Mwanza) na Rhino Rangers vs Polisi Tabora (Ali Hassan Mwinyi, Tabora).
 
Raundi ya pili ni Oktoba 27 mwaka huu; Polisi Tabora vs Polisi Dodoma (Ali Hassan Mwinyi, Tabora), Mwadui vs Polisi Mara (Kambarage, Shinyanga), Kanembwa FC vs Morani (Lake Tanganyika, Kigoma) na Pamba vs Rhino Rangers (Kirumba, Mwanza).
 
Oktoba 31 mwaka huu ni raundi ya tatu; Polisi Mara vs Rhino Rangers (Karume, Musoma), Morani vs Polisi Tabora (Kiteto, Manyara), Polisi Dodoma vs Pamba (Jamhuri, Dodoma) na Kanembwa FC vs Mwadui (Lake Tanganyika, Kigoma).

Monday, October 15, 2012

HASANOO NA KABURU WAULA PWANI


HASSAN Othman Hassan amechaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa Chama cha Soka Pwani (COREFA) huku nafasi ya katibu ikirudi tena kwa  Riziki Majala.

Naye Geofrey Irick Nyange amechaguliwa kuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu TF, Juma Haruna Kisoma Mwakilishi wa Klabu TFF na Abubakar Allawi  amechaguliwa kuwa Mhazini.

Waliochaguliwa kuwa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji katika uchaguzi huo uliofanyika kisiwani Mafia ni Musa Bakari Athumani, Godfrey Magnus Haule na Gwamaka Oden Mlagila na mwakilishi wa Wanawake ni Florence Ambonisye.


Akiongea na waandishi wa Habari Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Nchini(TFF) Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika juzi.

Pia aliongeza kuwa ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa COREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Pwani.

Pia alisema TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya COREFA chini ya uenyekiti wa Hassan Othman Hassan ambaye amechaguliwa tena kuongoza chama hicho.

Wambura alisema uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Pwani kwa kuzingatia katiba ya COREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.

"Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya COREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF", alisema Wambura.

13 WAPITISHWA KUGOMBEA TWFA

WAGOMBEA 13 kati ya 15 waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye Chama cha Soka la Wanawake Tanzania (TWFA) wamepitishwa baada ya usaili uliofanyika juzi.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA, Ombeni Zavala, waliopitishwa kwenye nafasi ya  Mwenyekiti ni Isabellah Husein Kapera, Joan Ndaambuyo Minja na Lina Paul Kessy.

Makamu Mwenyekiti ni Rose Kisiwa wakati wanaowania nafasi ya Katibu Mkuu ni Amina Ali Karuma na Cecilia Oreste Makafu.

Mgombea pekee wa nafasi ya Katibu Msaidizi, Macky Righton Mhango naye amepita kwenye usaili huo na kwenye nafasi ya Mhazini ni Rose Stewart Msamila.

Furaha Francis na Zena Chande wamepitishwa kuwania nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Soka nchini (TFF) wakati waliopita kuwania ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya TWFA ni Triphonia Ludovick Temba, Rahim Salum Maguza na Sophia James Charles.


Wagombea wawili ambao hawakupitishwa kwa ajili ya uchaguzi huo
unaotarajiwa kufanyika Novemba 4 mwaka huu ni Julliet Mndeme na Jasmin Soud walioomba ujumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF kwa sababu hawakufika kwenye usaili pia walikuwa wamewekewa pingamizi.

BONDIA WA TANZANIA MASHALI AMTWANGA MGANDA SEBYALA



 
Bondia Thomas Mashali usiku wa kuamkia leo alifanikiwa kumtupia makonde mazito na ya akili bondia Medy Sebyala wakati wa mpambano wao wa kugombea ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati ambapo Mashali alishinda kwa point.
 
Pichani juu akiwa na Kenyella mkuu wa jeshi la polisi Kinondoni

Picha ya kati akipambana vikali na mpinzani wake Medy Sebyala na picha ya chini akiwa na mashabiki wake akiwemo msanii wa muziki wa kizazi kipya Joseph Haule Profesa J, mlinzi wa kati wa mabingwa soka Tanzania Bara Simba, Juma Nyoso pamoja na kiungo Haruna Moshi 'Boban'.

ABDALLAH YUSUPH WA CLUB YA LUGALO ATWAA UBINGWA WA NMB MWALIMU NYERERE MASTERS GOLF




Mshindi wa mashindano ya gofu ya kumuenzi Mwl Nyerere Abdallah Yusuph toka klabu Lugalo akiwa na mgeni rasmi Jaji Mark Bomani na  Mkurugenzi wa wateja wakubwa wa benki ya NMB Kees Verbeek baada ya kutangwa mshindi kwenye hafla iliyofanyika juzi viwanja vya Gymkhana


Mashindando ya gofu ya kumuenzi Mwl JK Nyerere (Mwl Nyerere masters Golf) yaliyokuwa yanafadhiliwa na benki ya NMB  yaliyokuwa yanafanyika kwenye viwanja vya Gymkhana vya jijini Dar es salaam kuanzia jana yamefikia tamati leo kwa wachezaji mbalimbali kukabidhiwa zawadi zao huku mchezaji wa klabu ya Lugalo Abdallah Yusuph Idd akiibuka mchezaji wa jumla.

Mshiriki Abdallah Yusuph toka club ya Lugalo alitawazwa kuwa bingwa wa gofu ya kumuenzi mwalimu Nyerere mwaka 2012

Akifunga mashindano hayo ambayo yalikuwa yameshirikisha wachezaji zaidi ya 150 toka klabu mbalimbali za gofu Tanzania Mark Bomani ambaye ni Mkurugenzi wa bodi ya Kiwanda cha bia ya Serengeti alisema wachezaji wanatakiwa kumuenzi Mwl Nyerere kwa kuendeleza yale yote ambayo mwalimu aliyaacha.

Wachezaji wa umri mbalimbali kuanzia junior hadi elders walikabidhiwa zawadi zao,

Naye Mkurugenzi wa wateja wakubwa wa benki ya NMB Kees Verbeek alisema benki yake inafuraha kudhamini mashindano hayo kwa sababu inathamini yale ambayo mwalimu ambaye ni mwasisi wa taifa la Tanzania aliyoaacha kwani ndio maana na wao wanaweza kuwekeza maana mwalimu katuacha amani.

Nao wachezaji walioshiriki walisema mashindano yalikuwa mazuri na ushindani ni mkubwa kwani watu wameahamasika kujifunza kucheza gofu

Friday, October 12, 2012

VPL KUENDELEA KUTIMUA VUMBI KESHO

Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom inaendelea kesho  kwa timu kumi kupambana kwenye viwanja vitano tofauti katika raundi ya saba ya ligi hiyo yenye timu 14.
 
Polisi Morogoro itaikaribisha Azam kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro wakati mwamuzi wa FIFA, Oden Mbaga atakuwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya kuchezesha mechi kati ya wenyeji Tanzania Prisons na Oljoro JKT.
 
Jijini Tanga, Simba itakuwa mgeni wa Coastal Union kwenye Uwanja wa Mkwakwani katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka Pwani akisaidiwa na Godfrey Kihwili na Abdallah Uhako wote kutoka Arusha.
 
Mechi nyingine za kesho ni Ruvu Shooting dhidi ya African Lyon kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi, na Mtibwa Sugar watacheza na Mgambo Shooting kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani mkoani Morogoro.
 
Wakati huo huo, Azam imeomba mechi zake za nyumbani dhidi ya Yanga na Simba zichezwe kwenye uwanja wake wa Azam Complex ulioko Chamazi badala ya Uwanja wa Taifa.
 
Nayo Ruvu Shooting imeomba mechi yake ya ugenini dhidi ya Yanga ya Oktoba 20 mwaka huu ichezwe Uwanja wa Taifa badala ya Uwanja wa Azam Complex.
 
Maombi hayo yatawasilishwa kwenye kikao cha Kamati ya Ligi ya TFF kinachotarajiwa kufanyika kesho (Oktoba 13 mwaka huu) kwa ajili ya kufanyiwa uamuzi.
 
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)